Msaanii wa Bongo Muvi,Elizabeth Michael maarufu kama Lulu akiwa na wazazi waki wakiteta jambo na Wakili Peter Kibatala kabla ya shahidi amaye ni Daktari wa Hospitali ya Muhimbili kutoa ushahidiwake mbele ya mahakama kuu Kanda ya Dar es Salaam leo.

Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii.

MSANII maarufu wa filamu nchini, Elizabeth Michael maarufu kama Lulu, ameileza Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam  kuwa hakusababisha kifo cha marehemu Kanumba bali yeye ndiye aliyeshambuliwa.

Ameeleza kuwa kama siyo Kanumba kudondoka na panga kumtoka mkononi, basi yeye ndie angekuwa marehemu sasa hivi. Kwani kwa mwili wake mkubwa sikuweza kumfanya kitu chochote.

Lulu amedai hayo mbele ya Jaji Sam Rumanyika wakati akitoa utetezi wake katika kesi inayomkabili ya mauaji ya bila kukisudia dhidi ya msanii mwenzake, Marehemu Steven Kanumba, yanayodaiwa kutokea April 6, mwaka 2012 huko Sinza Vatkan.

Akiongozwa na wakili wa utetezi Peter Kibatala, Lulu amedai, mbali ya kuwa wanafanya kazi pamoja kama wasanii, pia alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Kanumba kwa takribani miezi minne kabla ya tukio kitokea.

Msaanii wa Bongo Muvi,Elizabeth Michael maarufu kama Lulu akipitia maelezo aliyochukuliwa na Polisi kipindi alipokamatwa ambayo aliyatoa kwaajili ya ushahidi kwa kuhusishwa na kifo cha Msanii Mwenzake Steven Kanumba. Maelezo hayo ameyapitia leo katika mahakama kuu ya Tanzania kanda ya Dar es Salaam. 

Akisimulia jinsi tukio zima lilivyotokea amedai, April 6 2012,  saa mbili usiku alienda nyumbani kwa rafiki zake mikocheni, akiwa huko Kanumba alikuwa akimpigia simu mara kwa mara kumuuliza mahali alipo. " sikimwambia nipo mikocheni maana mara nyingi alikuwa hapendi niwe mtu wa kutoka toka hasa kwenda sehemu za starehe bila yeye kiwepo". Amedai lulu.

Amedai baada ya kuona Kanumba anazidi kumpigia simu kumuuliza yuko wapi, aliamua kumwambia kuwa anataka kutoka ndipo akamwambia aende Sinza kumuaga.

Akadai alipita kumuaga na alipokaribia alimpigia simu kumwambia kuwa amekaribia kufika ndipo Kanumba alimwambia kuwa akifika aingie ndani moja kwa moja hadi ndani amemuachia mlango wazi.
"Niliingia ndani, nilimkuta anapaka Mafuta nywele zake akiwa kwenye dressing table na kwa kuwa chumbani hakukuwa na kiti nilipofika nilikaa kitandani tukasalimiana ambapo muda mfupi simu yake ikaita, alipokea na kuongea, " namalizia nakuja", nikajua anaongea na Chazi baba ndipo nami nikamwambia nataka kutoka"amedai lulu.

Ameendelea kudai, alipofika pale aligindua Kanumba ameishakunywa, akaniambia kama anatoka waende wote sehemu moja, akaongeza mara nyingi walipokuwa wakitoka wote sehemu moja kunatokea ugomvi, kwani ilipokuwa mtu akimsalimia akimkumbatia alikuwa akimpiga na pia walikuwa wanakwepa kwenda sehemu pamoja kwa ajili ya kukwepa vyombo vya habari.


BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...