Katibu Mkuu wa Yanga, Charles Boniface Mkwasa  akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam.

Klabu ya Yanga inatarajia kuwa ya pili kuingia katika mfumo wa hisa kutoka ule wa umiliki wa wanachama kama walivyofanya watani wao wa jadi Simba wiki mbili zilizopita.

Simba iliweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza Tanzania na Afrika Mashariki na kati kuingia mfumo huo ambapo Yanga wanatarajiwa kuwa wapili.

Katibu mkuu wa timu ya Yanga, Boniface Mkwasa amesema kikako cha kamati ya Utendaji kilichoketi Disemba 13 kimefikia maamuzi hayo ambapo watasubiri mkutano mkuu wa wanachama utakaofanyika ndani ya miezi mitatu ili kukamilisha jambo hilo.

Kocha huyo wa zamani wa timu ya taifa alisema wataunda kamati itakayosimamia mchakato wa zabuni ambao kwa mujibu wa katiba yao wanachama wanatakiwa kubaki na asilimia 51 na wawekezaji asilimia 49.

"Kamati ya utendaji imekutana juzi na kupitisha kubadili mfumo wa uendashaji wa klabu kutoka mfumo wa umiliki wa wanachama hadi hisa ambapo mchakato tayari umeanza siku chache zijazo tutatangaza kamati ya kusimama jambo hilo," alisema Mkwasa.

Simba iliingia rasmi kwenye mfumo wa hisa Disemba 3 mwaka huu ambapo mfanyabiashara Mohammed Dewji 'MO' alifanikiwa kushinda zabuni na atawekeza kiasi cha sh bilioni 20 kwa Wekundu hao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...