MWENYEKITI wa Chama cha Wananchi(CUF) Ibrahimu Lipumba amesema afya yake iko imara na hana tatizo lolote kiafya.
Ametoa
kauli hiyo muda huu wakati akizungumza na Michuzi Blog kwa njia ya
simu ambapo amesema anashangazwa na taarifa ambazo zipo kwenye baadhi ya
mitandao kuwa anaumwa na amelazwa Hospitali ya Agha Khan.
"Nimeshangaa
sana kusikia eti kuna taarifa zinadai nimepatwa na nshtuko, taarifa
hizo si za kweli na ndio hizo hizo zinaitwa feck news.Nipo imara na
najiandaa kwenda msikiti na baada ya hapo nitakwenda makao makuu ya
chama kwa ajili ya kusimamia kikao," amesema Prof Lipumba.
Amefafanua
hakuwa anajua kinachoendelea mtandaoni kuhusu yeye kwani anapoingia
kwenye mtandao ni kwa ajili ya kuangalia tafiti mbalimbali na si taarifa
za kuzusha.
Amesema
alishangaa kuona anapigiwa simu na watu mbalimbali wakimpa pole ya
ugonjwa ndipo aliposhangaa na kuanza kufuatilia chanzo cha hiyo taarifa.
Nimepata
fursa ya kuzungunza kwa kirefu na prof lipumba yupo bukheri wa afya
njema na ameshangazwa na uzushi kuwa ameptwa na mshutuko.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...