Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na mradi wa Little Hearts wa nchini Saudi Arabia ambao ni moja ya mradi wa Afya ulioko ndani ya Taasisi ya Msaada ya Muntada yenye makao Makuu yake mjini London nchini Uingereza zimefanya uchunguzi kwa watoto 131.

Uchunguzi huo umefanyika katika kambi maalum ya siku sita ya matibabu ya moyo kwa watoto wenye umri wa kuanzia mwaka mmoja hadi miaka kumi na nne ilianza tarehe 10/12/2017 na kumalizika leo tarehe 15/12/2017.

Kati ya watoto waliofanyiwa uchunguzi watoto 54 wamefanyiwa upasuaji wa bila kufungua kifua na 28 wamefanyiwa upasuaji wa kufungua kifua na hali zao zinaendelea vizuri. Kupitia kipimo cha kuangalia mtoto aliyepo tumboni kama anatatizo la moyo au (Fetal Echocardiography) tulimpima mama mwenye ujauzito wa miezi minne na kugundua kuwa mishipa ya damu ya mtoto imepishana. Mama huyu yuko chini ya uangalizi wetu hadi pale atakapojifungua.

Watoto waliofanyiwa uchunguzi na kufanyiwa upasuaji ni wale wenye matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo. Mioyo ya watoto hao ina matundu na mishipa ya damu ya moyo haipitishi damu vizuri.Changamoto kubwa tuliyokabiliana nazo katika kambi hii ni upatikanaji wa damu na ufinyu wa chumba cha uangalizi maalum (ICU) kwa wagonjwa ambao wanatoka katika chumba cha upasuaji.

Tunawaomba wananchi waendelee kujitokeza kwa wingi kuchangia damu. Mgonjwa anayefanyiwa upasuaji wa moyo anatumia kati ya chupa sita hadi saba za damu. Hivyo mahitaji ya damu ni makubwa kwa mgonjwa anayefanyiwa upasuaji wa Moyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...