Na Ismail Ngayonga
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa amewataka Watendaji wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo kutumia weledi, maarifa na ujuzi walionao ili kufanikisha adhma ya Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati kupitia uchumi wa viwanda.

Akizungumza katika kikao cha majumuisho ya Zaira yake ya kukagua miradi ya sekta ya ujenzi Mkoani Tanga na Watendaji wa Wizara hiyo, jana Alhamisi Februari 15, 2018, Naibu Waziri Kwandikwa amewataka Watendaji hao kubuni mipango na mikakati mbalimbali itayoweza kulisaidia Taifa.
Alisema  Watendaji wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo ikiwemo Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) na Wakala wa Ufundi na Umeme Serikalini (TEMESA) wana wajibu mkubwa wa kutimiza matarajio hayo yaliyowekwa na Serikali katika kufikia nchi ya kipato cha kati.
Kwa mujibu wa Kwandikwa alisema, Wizara hiyo imekuwa na watalaamu wa kutosha na wenye weledi ambao wamekuwa tegemeo kubwa katika Taifa, hivyo ni wajibu wa Watendaji hao kufanya kazi kwa bidii kwa kutumia vipaji vyao badala ya kuacha ujuzi na maarifa waliyonayo yakipotea bila ya kuinufaisha.
“Wizara hii, imekuwa tegemeo katika sekta zote za kiuchumi, hususani wahandisi tulionao katika Taasisi zetu, hivyo ni vyema tuhakikishe kuwa utaalamu huu unaweza kuleta matokeo chanya katika Taifa letu ikizingatia kuwa Tanzania ya Uchumi wa Viwanda itagemea sana Wataalamu wengi kutoka Wizara yetu” alisema Kwandikwa.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa akisalimiana na Watendaji wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo ikiwemo TBA, TANROADS na TEMESA wakati wa mkutano wa majumuisho ya ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya sekta za ujenzi inayosimamiwa na Wizara hiyo jana Alhamisi Februari 15, 2018. Kulia kwake ni Meneja wa TANROAD Mkoa wa Tanga, Mhandisi Alfred Ndumbaro.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa akizungumza na Watendaji wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara hiyo ikiwemo TBA, TANROADS na TEMESA wakati wa mkutano wa majumuisho ya ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya sekta za ujenzi inayosimamiwa na Wizara hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...