Na Karama Kenyunko, blogu ya jamii.

MAHAKAMA nchini Tanzania, imewataka madalali wa Mahakama kuwa na cheti cha umadhubuti katika kazi hiyo toka Chuo cha Uongozi wa Mahakama ama Taasisi inayotambuliwa na kamati ya uteuzi.

Jaji kiongozi wa Mahakama ya Tanzania, Frerdnand Wambali amesema haya leo jijini Dar es Salaam wakati wa ufunguzi wa kongamano la wadau mbalimbali wa Mahakama wanaoratibu na kusimamia utekelezaji wa amri za mahakama wakiwamo madalali.

Lengo la kongamano hilo ni kujadili rasimu ya mtaala maalumu wa kutolewa mafunzo kwa watu wanaofanya shughuli za udalali na usambazaji wito na amri za Mahakama.

Kongamano hilo limeratibiwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama Rushoto kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania lengo ni kujadili rasimu ya mtaala maalum wa kutolewa mafunzo kwa watu wanaofanya shughuli za udalali na usambazaji wito na amri za Mahakama.

Akizungumza, Jaji Wambali amesema Mahakama inatambua madalali wa Mahakama na wale wanaopaswa kupelekwa hati za kuitiwa kwenye mashauri wanawajibu wa kuhakikisha amri mbalimbali zinazotolewa na mahakama hasa katika mashauri ya madai zinatekelezwa kwa mujibu wa sheria na kanuni zilizowekwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...