Na Agness Francis Globu ya jamii
MABINGWA watetezi Tanzania Bara Yanga SC wanashuka dimbani Stade Linite kufuana na mabingwa wa Shelisheli St. Lous kwenye Michuano ya klabu Bingwa Barani Afrika.
Mtanange huo utakaopigwa saa za Afrika Mashariki 10 jioni ambapo ni mchezo wa marudiao baada ya kushinda bado 1-0 wiki iliyopita katika dimba la Uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam.
"Tumejipanga vema kushinda mchezo wa leo nimewapanga vijana kuwa makini dakika zote 90,lakini nimewaambia kuwa makini na dakika 20 za mwanzo tutajitahidi kushinda na kumiliki mpira",amesema Lwandamina.
Aidha wachezaji watakaoukosa mchezo huo wachezaji wake mahiri Obrey Chirwa ambaye aliumia goti katika mchezo wao uliopita dhidi ya MajimajiFc, Thabani Kamusoko, Donald Ngoma, Yohana Nkomola pamoja na Hamisi Tabwe ambao wanaendelea na mazoezi binafsi baada ya kupona majeraha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...