Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
Jamii imetakiwa kulifahamu vyema tatizo la kifua kikuu na kushirikiana na Wizara ya afya kupitia Kitengo shirikishi cha UKIMWI, Homa Ya Inni, Kifua kikuu na Ukoma ili kukabialiana na tatizo hilo.

Wito huo umetolewa na Waziri wa Afya Hamad Rashid Mohammed alipokuwa akizungumza na Wanahabari ofisini kwake Mnazimmoja mjini Zanzibar kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya Kifua kikuu duniani.

Amesema Maradhi ya Kifua kikuu, ni moja kati ya maradhi ambayo Shirika la afya Duniani limeyapa kipaumbele ili kuweza kufanikisha mapambano dhidi yake.

Waziri Hamad amesema kila ifikapo Machi 24 ya kila mwaka ndiyo siku ya maadhimisho ya  Kifua Kikuu ulimwenguni ambapo hutumika kuikumbusha  na kuishajihisha jamii kuwa Kifua Kikuu bado ni janga kubwa katika jamii.

Aidha kupitia maadhimisho hayo Wizara ya afya ikishirikiana na Viongozi mbali mbali huitumia fursa hiyo kutathmini juu ya hali ya maradhi nchini na kuandaa mikakati madhubuti ya kupambana nayo.
  Msaidizi Meneja kitengo shirikishi Ukimwi,Kifua kikuu na Ukoma Issa Abeid akizungumza machache na kumkaribisha Waziri wa afya Hamad Rashid Mohamed kuzungumza na waandishi wa habari  kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku hiyo.
 Meneja kitengo shirikishi Ukimwi,Kifua kikuu na Ukoma Farhat Khalid akitoa ufafanuzi namna ya kupunguza maambukizi ya Kifua Kikuu.
 Waziri wa afya Zanzibar, Hamad Rashid Mohammed akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali hawapo pichani kuelekea  katika kilele cha maadhimisho  ya  siku ya Kifua Kikuu.
 Mwandishi wa habari wa ITV na Radio ONE, Farouk Karim akiuliza maswali katika mkutano huo.
Naibu Waziri wa Afya Zanzibar, Harusi Said Suleiman akitoa shukurani kwa waandishi wa habari na wadau mbalimbali waliojitokeza katika mkutano huo.(Picha na Abdalla Omar Maelezo – Zanzibar).

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...