Wananchi mkoani Dodoma wameendelea kufurika kwenye vituo vya Usajili mkoani humo kushiriki zoezi la Usajili wa Vitambulisho vya Taifa linaloendeshwa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa- NIDA.

Zoezi hilo ambalo limelenga kuwasajili wananchi wote wenye umri wa miaka 18 na kuendelea limeonekana kuwavuta wananchi kwa wingi tofauti na ilivyokuwa siku za nyuma wakitokea maeneo mbalimbali ya mkoa huo na viunga vyake.

Kata ya Chamwino na Chang’ombe zilizopo Wilaya ya Dodoma mjini leo zimetia fora kwa maelfu ya wananchi waliomiminika alfajiri kupata huduma hiyo huku baadhi wakionekana kwenye mitaa ya mji huo wakihaha kutoa nakala (copy) ya viambatisho vyao kwenda kujaza fomu.
Akizungumzia mwenendo wa zeozi hili ambalo lilianza tangu mwezi Februari,2018; Mtendaji wa Kata ya Chang’ombe Bi. Neema Makinda amesema mwitikio wa watu ni mkubwa na wamejipanga kuwahudumia wananchi wote wa Kata hiyo ambao idadi yao ni Zaidi ya elfu 25.
 Mtendaji  wa Kata ya Chang’ombe Bi. Neema Makinda akimpitishia fomu mmoja wa wananchi wa Kata hiyo aliyefika kwenye kituo cha Usajili kusajiliwa.
 Bw. Jumanne Bakari akikaguliwa fomu yake na Mwenyekiti wa Mtaa wake Bi. Havijawa Ramadhani ( wa kwanza kushoto) na pembeni yake ni Bi. Tatu Kimwaga mjumbe wa Mtaa.
 Baadhi ya wananchi wa Kata ya Chamwino wakiwa wamejipanga kwenye foleni  kwenye viwanja vya wazi nje ya Shule ya Msingi Chamwino wakisubiri kusajiliwa  Vitambulisho vya Taifa.
 Bi. Asha Twaha Mruma, mwananchi katika Mtaa wa Chamwino akiwa anajaza fomu ya maombi ya Vitambulisho vya Taifa huku pembeni mtoto wake mdogo wa kiume akishuhudia mama yake akijaza fomu hiyo kwa umakini mkubwa.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...