Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini .

CHUO kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) kimezundua zoezi la upimaji wa Homa ya Ini kwa Watumishi ,Wategemezi wao pamoja na majirani wa cuo hicho ikiwa ni njia ya tahadhari licha ya kutokuwepo ushahidi wa mlipuko wa ugonjwa huo nchini. 

Serikali inatambua umuhimu wa afya bora kwa watumishi wake kwani afya bora ni rasilimali muhimu kwa maendeleo na maenedeleo ya Taifa yataletwa na wananchi pamoja na watumishi wenye Afya na wenye uwezo wa kuzalisha mali na kutoa huduma stahiki kwa umma wa Tanzania. 

Katika kuzingatia sera na miongozo ya Afya ya mwaka 1990 iliyopitiwa mwaka 2007 ,Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MOCU) kama mdau imeanza kutoa huduma ya upimaji wa Ini kupitia Kituo chake cha Afya kilichopo chuoni hapo. 
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Mosi (MoCU) Prof ,Faustine Bee akizungumza wakati wa uzinduzi wa Upimaji wa Homa ya Ini kwa Watumishi wa Chuo hicho pamoja na Wategemezi wao, zoezi ambalo linafanyika katika kituo cha Afya kilichopo chuoni hapo . 
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) ,Eustace Ng'weshemi akizungumza wakati wa uzinduzi wa zoezi la upimaji wa Homa ya Ini katika Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi .
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) Dkt , Eustace Ngw'eshemi akimuonesha Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi ,Prof Faustine Bee namba ya siri itakayotumika wakati wa kupokea majibu baada ya zoezi la upimaji kukamilika.
Mkuu wa kitengo cha Maabara katika Kituo cha Afya cha Chuo Kikuu cha Ushirika (MOCU) Aniseth Malenga akivuta Damu katika mkono wa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika ,Prof Faustine Bee alipoongoza zoezi la upimaji wa Homa ya Ini kwa watumishi wa chuo hicho.
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya cha Chuo Kikuu cha Ushirika ,Moshi (MoCU) Dkt , Eustace Ngw'eshemi akizungumza na mmoja wa watumishi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi kabla ya kumfanyia vipimo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...