Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

KATIKA kuadhimisha Siku ya kimataifa ya mtoto wa kike kampuni ya simu ya Airtel Tanzania sambamba na Chuo cha Mafunzo ya Ufundi(VETA), wamekuja na mbinu mpya ya kutoa mafunzo kupitia simu ya mkononi.

Akizungumza na Michuzi blog Meneja mradi wa Airtel Jane Matinde ameeleza leo jijini Dar es Salaam kwa kushirikiana na VETA wameamua kutoa mafunzo ya nadharia na vitendo kupitia apllication ya Vsomo inayopatika playstore bure kabisa ambayo baada ya kusoma ukifaulu kwa asilimia 40 atachaguliwa katika VETA iliyokaribu kuweza kuendelea na masomo.

Aidha ameeleza zaidi ya kozi 11 zinapatikana, hivyo vijana wanatakiwa kupakuwa application hiyo ili kujifunza kozi mbalimbali kama vile umeme wa majumbani na malipo ya kozi hizi ni shilingi laki moja na ishirini pekee.Kwa upande wa Meneja mradi wa Vsomo kutoka VETA Charles Mapuli ameeleza hadi sasa waliopakua application hiyo wapo zaidi ya 3500, waliosajiliwa 10,800 na waliosoma na kufanya mitihani wapo 120.

Pia masomo hayo ni ya muda mfupi kwa miaka miwili hadi mitatu na itawasaidia vijana wengi kufikia malengo yao na kufikia azma ya serikali ya kujenga Tanzania ya viwanda.

Meneja mradi wa Airtel Jane Matinde akizungumza na Michuzi blog leo jijini Dar es salaam kuhusiana na fursa ya Vsomo ambaye inatoa fursa ya kusoma masomo ya ufundi kupitia simu ya mkononi.
Katibu mkuu Wizara ya Elimu Dkt. Ave Maria Semakafu akisikiliza maelezk kutoka kwa Meneja mradi wa Airtel Jane Matinde kuhusiana na kusoma kupitia simu ya mkononi maarufu kama VSOMO.
Baadhi ya wanafunzi wakimsikiliza meneja wa Vsomo,Charles Mapuli kutoka VETA katika maonesho ya siku ya kitaifa ya mtoto wa kike na Tehama leo jijini Dar es salaam.(Picha na Emmanuele Massaka,Globu ya jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...