Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
JAMII imeaswa kujenga misingi imara ya malezi ya  watoto ili wasiweze kuishi maisha ya mitaani na ambayo yanasababisha kokosa haki za kupata elimu pamoja na malezi mengine.

Hayo ameyasema leo Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Sihaba Nkinga wakati akizindua ripoti ya Taifa ya Watoto wanaoishi na kufanya Kazi Mitaani nchini Tanzania, amesema kuwa sehemu salama ya kuishi watoto ni katika familia au jamii.

Amesema kuwa katika ripoti hiyo watoto wa kike wamekuwa wakionekana katika majira ya usiku wakijiuza huku watoto wakiume wanaonekana majira ya mchana na usiku.

Nkinga amesema kuwa serikali itafanyia kazi mapendekezo ya ripoti hiyo ili katika kuweza kuhakikisha watoto hao wanakwenda katika familia zao.

Amesema sababu zinazowafanya watoto kuishi na kufanya kazi mitaani  ni umasikini pamoja na ukatili wa kupindukia na kuamua baadhi ya watoto kutoroka katika familia zao na kuingia mitaani.

“Jamii iendelee  kuishi kwa amani na misingi bora katika malezi ya watoto katika kuhakikisha hawakimbilii mitaani kwa kuishi kwa kukosa chakula, elimu pamoja wengine kupoteza maisha kutokana na kupigwa “amesema Nkinga.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Sihaba Nkinga akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti ya Taifa ya Watoto wanaoishi na kufanya Kazi Mitaani nchini Tanzania uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Sihaba Nkinga akikata utepe kuashiria uzinduzi wa ripoti ya Taifa ya Watoto wanaoishi na kufanya Kazi Mitaani nchini Tanzania uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Railway Afrika, Peter Kent akizungumza na waandishi wa habari juu ya mikakati ya shirika hilo katika masuala ya watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani wakati wa uzinduzi wa ripoti ya Taifa ya Watoto wanaoishi na kufanya Kazi Mitaani nchini Tanzania uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
 Naibu Mwakilishi Mkazi USAID Kizazi Kipya Project wa PACT Tanzania, Levina Kikoyo akizungumza jinsi ya utafiti waliofanya katika ripoti hiyo.
 Sehemu ya wadau mbalimbali wa masuala ya watoto waliohudguria katika uzinduzi wa ripoti ya Taifa ya Watoto wanaoishi na kufanya Kazi Mitaani nchini Tanzania uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Sihaba Nkinga akiwa na wawakilishi wa mashirika wakati wa uzinduzi ya Taifa ya Watoto wanaoishi na kufanya Kazi Mitaani nchini Tanzania uliofanyika leo jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...