KAMPUNI ya Mipango Miji na Vijiji inayotoa ushauri elekezi kuhusu ardhi (HUSEA), imeunga mkono kauli ya Rais Dk. John Magufuli ya kuhamishia shughuli za mipango miji na kuzipeleka wizarani badala ya Tamisemi.

Wiki iliyopita Rais Magufuli aliagiza watalaamu wote wa ardhi na mipango miji katika halmashau zote nchini kusimamiwa moja kwa moja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana Mwenyekiti wa kampuni hiyo Renny Chiwa alisema kuwa uamuzi huo utasaidia kuboresha utendaji wa kazi za mipango miji.

"Tunampongeza Rais Magufuli kuhamisha shughuli za mipango mini wizarani Kwa sababu kuna watalamu was fani hiyo wanaweza kusimamia vizuri kuliko ilivyokua awali," alisema Chiwa.

Alisema uamuzi wa rais ni kutaka kuboresha shughuli za mipango miji pamoja na kuwawajibisha watendaji ambao watashindwa kutimiza majukumu yao ipasavyo.Alisema kutokana na hali hiyo mabadiliko hayo yanaweza kuleta tija na nchi kuwa na mipango bora ya ardhi itakayotoa sura mpya.

Alisema kimsingi wataalamu wa ardhi na mipango miji katika halmashauri ni sawa na watumishi wengine katika serikali za mitaa, kwani wamekuwa wakiwajibika kiutawala moja kwa moja kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali na Serikali za Mitaa (TAMISEMI). 

Alisema kumekuwepo na changamoto za kiutendaji ambazo zinahitaji watalaamu was fani hiyo kukaa na kubuni mipango thabiti ya ardhi, hivyo basis ni vema suala hill litasimamiwa na watalaamu wenye fani hiyo.Alisema kutokana na hali hiyo mabadiliko hayo yataimarisha usimamizi wa idara husika ya ardhi na mipango miji katika halmashauri.

Alisema kutokana na hali hiyo watalaamu watakapkuwa katika kitengo hicho wanapasww kufanya kazi zao Kwa weledi ili wasimuangushe Rais.“HUSEA tunaona kuwa uamuzi huu wa Rais utazidi kuongeza ufanisi na kasi ya utekelezaji wa urasimishaji makazi nchini ambayo wizara hiyo yamekuwa yakitekelezwa kwa pamoja chini ya msukumo mkubwa wa Waziri wa wizara hiyo, William Lukuvi.
pichani kushoto ni Mratibu wa miradi wa kampuni ya mipango miji ya Husea,Edward Kinabo,Mwenyekiti wa kampuni Renny Chiwa pamoja na  Mkuu wa idara ya mipango miji na vijiji wa kampuni hiyo Aloyce Nyaisa,wakiunga mkono uamuzi wa serikali wa kuhamisha shughuli za mipango miji kutoka Tamiseni na kuzirudisha wizarani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...