Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kulia) akizungumza na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Bw. Alvaro Rodriguez alipofika Wizarani tarehe 11 Juni, 2018 kwa ajili ya kuzungumzia masuala mbalimbali kuhusu ushirikiano kati ya Umoja wa Mataifa na Serikali ya Tanzania pamoja na utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDG's) hapa nchini. Kwa upande wake, Prof. Mkenda alipongeza Mpango wa One UN unaotekelezwa na Ofisi za Umoja wa Mataifa hapa nchini kwa vile unarahisisha utekelezaji wa majukumu na kushukuru ushirikiano mzuri uliopo kati ya Umoja wa Mataifa na Tanzania hususan katika program za kupunguza umaskini na maendeleo endelevu. 
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimatifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Celestine Mushy akiwa na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Eva Ng'itu wakifuatilia mazungumzo kati ya Prof. Mkenda na Bw. Rodriguez hawapo pichani 
Bw. Rodriguez nae akimweleza jambo Prof. Mkenda 
Mazungumzo yakiendelea 
Picha ya pamoja 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...