Na Frankius Cleophace, Musoma.

Wafanyabiashara wa Madini kutoka Migodi mbalimbali ya Dhahabu Mkoani Mara wameondokana na adha waliyokuwa wakiipata ya kusafirisha Mchanga wa dhahabu kwaajili ya kuchenjua Mkoani Mwanza kabla ya katazo la serikali baada ya kufunguliwa kwa kiwanda cha FRAMAL INVESTMENT LTD Manispaa ya Musoma mkoani Mara kwaajili ya uchenjuaji wa dhahabu.

Mmilikiwa kiwanda hicho FRANK MALIMA anasema awali alikuwa na kiwanda Mkoani Mwanza lakini baada ya Serikali kuzuia usafirishaji wa Mchanga wa Dhahabu kutoka Mkoa mmoja hadi mwingine ameamua kufungua kiwanda Mkoani Mara kwaajili ya kutoa huduma kwa wafanyabiashara wa Madini.

Frank amesema kuwa Mkoa wa Mara unazalisha sana Dhahabu hivyo ameamua kufungua kiwanda hicho kwa lengo la kutekeleza Serikali ya Viwanda ikiwa ni pamoja na kuwasaidia Wafanyabiashara hao.

Ameongeza kuwa Kwasasa kiwanda hicho kina uwezo wa kuchenjua tani 1.5 ya Dhahabu kwa saa 24 hatua ambayo Mmiliki huyo amesema bado kumeonaka kuwepo na upungufu wa Mashine hizo na hivyo kuwa katika harakati za kutengeneza Mashine zingine ambazo anaamini zitasaidia kukidhi Mahitaji.

Nao baadhi ya wafanyabiashara wa Madini wakatoa pongezi kwa Mmiliki wa kiwanda hicho na kusema kulikuwa na changamoto kubwa kabla ya kuwepo kwa kiwanda hicho.
Mitambo kwa ajili ya Uchenjuaji wa Dhahabu katika Kiwanda hicho kilichopo Mjini Musoma Mkoani Mara.
Mkurugenzi wa Kiwanda cha FRAMAL INVESTMENT LTD Frank Malima akionyesha baadhi ya Mitambo katika Kiwanda hicho
Gari la kampuni hiyo ambalo linafanya hughuli za Usafirishaji wa Mchanga huo.
Mkurugenzi wa Kiwanda hicho akiongea na Vyombo vya habari ofisini Kwake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...