Said Mwishehe,Globu ya jamii
BENKI ya Biashara Dar es Salaam(DCB) imetangaza kupata faida ya Sh.bilioni moja katika kipindi cha nusu ya kwanza ya mwaka 2018 ambacho kimeishia Juni.

Akizumgumza leo Dar es Salaam Mkurugenzi wa Fedha wa DCB Zacharia Kapama amesema faida hiyo ni ongezeko la asilimia 106 kutoka faida ya kipindi kama hicho kwa mwaka 2017.

"Ongezeko hilo la faida pia lilipatikana kutokana na kuimarika kwa mapato yatokanayo na riba pamoja na yale yasiyotokana na riba.

"Na limechagizwa na mkazo wa benki katika amana za gharama nafuu, usimamizi wa mizania wenye ufanisi, ufunguaji wa tawi la Dodoma na vituo vya huduma, ukuaji wa mfumo wa kibenki wa kidijitali na wa mawakala pamoja na ongezeko la wateja na miamala,"amesema.

Kapama amesema pia mafaniko hayo yametokana na ukuaji wa mikopo ambapo benki hiyo imefanikiwa kuongeza kiwango cha mikopo kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na mikopo iliyokuwepo katika Desemba mwaka 2017.

Pia amesema ufanisi wa benki hiyo umeongezeka hasa katika usimamizi wa matumizi ya riba na yasiyo ya riba, ufanisi wa mizania na uboreshaji wa huduma za utoaji wa mikopo.

Amefafanua katika utoaji huduma, benki ya biashara ya DCB imefanikiwa kuongeza idadi ya wateja kufikia 191,133 katika nusu ya pili ya mwaka iliyoishia Juni mwaka 2018 kutoka 188,305 Desemba mwaka 2017.

"Ongezeko hili la wateja 2,828, limechangia kuimarisha mapato ya benki kupitia kuongezeka kwa miamala, amana za kudumu na utoaji mikopo.
Mkuu wa Idara ya Fedha wa Benki ya Biashara ya DCB, Zacharia Kapama (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo wakati benki hiyo ikitangaza faida ya Sh.bilioni 1.0 katika kipindi cha nusu ya kwanza ya mwaka 2018. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano Rahma Gemina na kushoto ni Mkaguzi Mkuu wa ndani Deogratias Thadei.

 KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...