Viongozi wa serikali nchini Kenya wameomba kuendelea kushirikiana vyema na serikali ya Tanzania katika kupinga na kupiga Vita suala la Ukeketaji kwa Watoto wa kike huku serikali ikiongoza vyema wazee wa mila baina ya nchi hizo mbili bila kutumia nguvu kwa lengo la kutokomeza Mila na desturi ambazo zimepitwa na wakati ukiwemo Ukeketaji ambao ni chanzo kikubwa cha ndoa za Utotoni.

Zacharia Marwa ni katibu wa Muungano wa koo ya Kurya nchini Kenya na Tanzania anabainisha hayo katika Mkutano wa hadhara uliofanyika maeneo ya Gokeharaka Kurya Mashariki nchini Kenya kwa kukutanisha wazee wa mila Muungano wa koo 12 wilaya ya Tarime pamoja na wazee wa mila koo 4 nchini Kenya.

Zacharia amesema kuwa ili kukomesha Ukeketaji Viongozi wa Tanzania na Kenya waendelee kushirikiana Vyema na wazee wa Mila kutoka Muungano wao bili kutumia nguvu huku elimu ikiendelea kutolewa katika jamii juu ya madhara ya ukeketaji kwa motto wa kike.
Katibu wa Muungano wa wazee wa Mila nchini Kenya, Zacharia Marwa (aliyesimama kulia) akifafanua jambo kwa Wazee wa Mila kutoka Tanzania na Kenya katika Eneo la Gokeharaka Kurya Mahariki nchini Kenya.
Irene Mukanzi ambaye ni Afisa taara ya Kehancha katika Wilaya ya kuria Magharibi akiongea na Wazee hao ambapo amesema kuwa Sheria za kupinga Ukeketaji Nchini Kenya zinaendelea kufanya kazi.
Magoko Maroa ambaye ni Chief Gokeharaka Mashariki mwa Kenya akingea na Wazee hao.
Sammy Chacha ambaye ni Chief Bukira South nchini Kenya akiongea na Wazee wa mila katika Kikao hicho cha pamoja.
Sister Stella Mgaya ambaye ni Mkurugenzi wa shirika la ATFGM Masanga Wilayani Tarime nchini Tanzania ambao wanapiga vita ukatili wa kijinsia ukiwemo ukeketaji akiongea na wazee wa Mila pande zote mbili Tanzania na Kenya na kusema kuwa baada ya kutoa Elimu ya kupinga Ukeketajia sasa wameamua kwenda nchini Kenya lengo likiwa ni kuokoa Mtoto wa Kike.
Wazee wa Mila Muungano wa koo12 Tarime nchini Tanzania wakiwa katika kikao cha pamoja na wazee wa Mila koo 4 nchini Kenya eneo la Gokeharaka Kurya Mashariki Nchini Kenya lengo ni kuzungumzia suala la kupiga Vita Ukeketaji kwa Mtoto wa kike. Habari/Picha na Na Frankius Cleophace, KENYA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...