Na Rashid Nchimbi wa Polisi Arusha

Wananchi wa mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One jijini hapa, wametakiwa kuendeleza ushirikiano uliopo baina yao na kikundi cha ulinzi shirikishi ili kuweza kuimarisha usalama katika eneo lao.

Wito huo ulitolewa jana jioni na Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng’anzi wakati alipokuwa anafunga mafunzo ya wiki mbili ya kikundi cha ulinzi shirikishi cha mtaa huo pamoja na kuwapa vitambulisho askari 16 waliopewa mafunzo hayo.

Kamanda Ng’anzi alisema mbali na askari wa kikundi hicho kufanya doria katika eneo hilo pia watahitaji kupata taarifa za uhalifu toka kwa wananchi ili waweze kubaini maeneo korofi ambapo kama zitakuwa juu ya uwezo wao watashirikiana na Jeshi la Polisi.

Aidha aliwataka askari hao kufanya kazi kwa kufuata taratibu kama jinsi walivyoelekezwa katika mafunzo yao na kutomuonea mtu yoyote hali ambayo itasidia kuimarisha mahusiano bora baina yao na wananchi.

Hata hivyoKamanda Ng’anzi  aliwataka wananchi hao nao pia wawe mstari wa mbele katika jukumu la ulinzi badala ya kutegemea baadhi ya vyombo vya ulinzi pekee kwani Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imewapa dhamana.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng'anzi akimpa kitambulisho mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Polisi Jamii wa Mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One jijini Arusha.
Meya wa Jiji la Arusha Bw. Kalist Lazaro akiongea na wananchi wa mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One kabla Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha kufunga rasmi mafunzo ya kikundi cha ulinzi shirikishi cha mtaa huo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ramadhani Ng'anzi pamoja na wageni wengine wakiwa katika picha ya pamoja na askari wa kikundi cha Ulinzi Shirikishi cha Mtaa wa Kanisani kata ya Sokoni One kilichopo jijini Arusha. (Picha na Rashid Nchimbi wa Polisi Arusha).

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...