*Ni ishara ya kumuombea dua kwa Mungu,pia kumshukuru kwa kusaidia kutatua kilio chao

MKAZI wa Kijiji cha Kidoka Wilaya ya Chemba, Roza Mkali ameamua kumshika  kichwa mdau wa  maendeleo wa wilaya hiyo, Khamis Mkotya, ikiwa ni ishara ya kumwombea dua.

Pia ikiwa ni  kumshukuru baada ya kufanikisha familia hiyo na nyingine zaidi ya tano kijijini hapo kulipwa fidia ya mashamba yao yaliyokuwa yamechukuliwa na mkandarasi wakati wa ujenzi wa barabara ya Dodoma - Babati.  

Imeelezwa kuwa  wananchi hao walikata tamaa mwishoni mwa mwaka juzi kutokana na kufuatilia malipo yao bila mafanikio. Hivyo Mkotya aliguswa na kero hiyo hivyo aliamua kushirikiana nao na kuwapigania hadi walipolipwa stahiki zao. 

Juzi wakati Mkotya akitoka Dodoma kwenda Kondoa aliamua kupita kijijini hapo ndipo familia hiyo ilipomkaribisha nyumbani ili aone matunda ya kazi yake ya kuwapigania.

 Familia hiyo ilimweleza Mkotya kuwa inayofuraha kubwa kwani fedha walizopata wameweza kununua mashamba mengine na kujenga nyumba bora ya bati.
 MKAZI wa Kijiji cha Kidoka Wilaya ya Chemba, Roza Mkali akiwa amemshika kichwa mdau wa  maendeleo wa wilaya hiyo, Khamis Mkotya, ikiwa ni ishara ya kumwombea dua.
 Mdau wa Maendeleo wilaya ya Chemba,Hamis Mkotya akizungumza jambo na Mkazi wa kijiji cha Kidoka Wilayani Chemba,Roza Mkali hivi karibuni mara baada ya tatizo walilokuwa nalo kutatuliwa

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...