Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imetoa siku saba kwa upande wa mashtaka kukamilisha mchakato wa kubadilisha hati ya mashtaka kwa kuwaondoa Zacharia Hans Poppe na Franklin Lauwo ili kesi dhidi ya washtakiwa Evans Aveva na Godfrey Nyange iweze kuendelea.

Amri hiyo, imetolewa leo na Hakimu Mkazi Mkuu,Thomas Simba baada ya Wakili wa Takukuru, Leonard Swai kueleza mahakamani hapo kesi imepangwa kwa ajili ya kutajwa na washtakiwa Aveva na Nyange wapo mahakamani.

Amedai mara ya mwisho Mahakama ilitoa agizo la kuwaondoa Poppe na Lauwo katika hati ya mashtaka ili kesi iendelee kwa Aveva na Nyange.
Amedai utaratibu umefanyika na jalada limepelekwa kwa DPP na amejitahidi kulifuatilia hadi leo asubuhi na ametoka kwa DPP lakini hajaweza kulishughulikia, yupo nje ya Dar es Salaam.

Kutokana na hali hiyo ameomba Mahakama wapewe wiki mbili kwa ajili ya kuhakikisha DPP analifanyia kazi hata kama atakuwa Dodoma watamfuata huko huko.Baada ya Hakimu Swai kueleza hayo, Aveva aliomba wapewe muda wa siku saba kwa sababu siku 14 ni nyingi na kuongeza kuwa upande wa mashtaka wanavyochelewesha jambo hilo wanawaumiza.

Pia Nyange ameongeza kuwa jambo hilo la kubadilisha hati ya mashtaka kwa kuwaondoa washtakiwa hao ni la muda wa zaidi ya miezi miwili wakati wanajua wapo mahabusu kwa zaidi ya mwaka mmoja na kuendelea kukaa huko ni tatizo.Amesisitiza kuwa kuendelea kuwapatia upande wa mashtaka wiki mbili ni kama kuendelea kuwaficha Keko bila sababu za msingi.

Baada ya malalamiko hayo ya washtakiwa Hakimu Simba alimuuliza Wakili Swai unaona malalamiko ya washtakiwa hayana msingi. Swai akamjibu Hakimu Simba kuwa malalamiko yao yanamsingi mheshimiwa.Hakimu Simba unasemaje na afya ya mshtakiwa wa kwanza Aveva inaonekana ana kliniki kila wiki hivyo anawapa siku saba wakamilishe taratibu. Kesi imeahirishwa hadi Agosti 17 mwaka 2018

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 10 yakiwemo ya kula njama, kughushi, kuwasilisha nyaraka za kughushi, kutoa maelezo ya uongo na utakatishaji fedha haramu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...