Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF)leo Jumanne Septemba 4,2018 limemtangaza Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Dkt Reginald Mengi kuwa mlezi wa timu ya Taifa ya Vijana U17 "Serengeti Boys"

Dkt Mengi amekuwa akiifuatilia kwa karibu timu hiyo na amekuwa mmoja wa wadau wakubwa wa soka la Vijana.  Akiwa 

ni mpenda maendeleo ya mpira wa Miguu hususani soka la Vijana na amekuwa shabiki mkubwa wa Serengeti Boys.

TFF tunaamini tutashirikiana vizuri na Dkt  Mengi katika maendeleo na ustawi wa soka la Vijana na ni mwanamichezo ambaye hakika amekuwa mstari wa mbele katika kukuza na kuendeleza soka la Vijana. 

Mara kadhaa amekuwa akiwasiliana na TFF kufuatilia maendeleo ya timu ya Taifa ya U17 kwenye mashindano mbalimbali. 

TFF wamefarijika kwa Dkt Mengi kukubali kuwa mlezi wa timu hii ya Serengeti Boys na wanaamini kwa pamoja wataifanya timu hii kuwa msingi mzuri katika maendeleo ya ustawi wa soka la Vijana. 


Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP Ndugu Reginald Mengi .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...