JESHI la Wananchi wa Tanzania JWTZ Leo limeadhimisha miaka 54  tangu kuanzishwa kwake.

Maadhimisho hayo yamefanyika jijini Dar es salaam chini ya Mkuu wa Majeshi Generali Venance Mabeyo akiwa na mgeni rasmi mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda, kwa kufanya usafi katika eneo la kambi ya Jeshi Lugola na  baadaye kufuatiwa na michezo iliyofanyika katika eneo la Uwanja wa Jeshi mwenge vinyago .

Akizungumza katika maadhimisho hayo mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amelipongeza Jeshi hilo kwa kudumisha usafi na kuwataka wananchi wa mkoa huo kuiga mfano wa Jeshihilo kutumia mazingira kwa usafi na kupanda miti katika maeneoyao.

Aidha Makonda ameelezeakusikitishwa kwake na kitendo cha mgambo wanaosimamia usafi katika jijini la Dar es salaam kwenda kinyume cha sheria katika kusimamia zoezi hilo kwakupiga wananchi na kusema kuwa hajawatuma kufanya hayo  na ametoa amri wakamatwe .

''Sheria zipo hakuna hata mmoja inayosema adhabu ya kukutwa na uchafu ni kupigwa bali sheria imeongelea faini, nimeagiza tangu jana walihusika na hilo tukio wakamatwe na hatua za sheria zichukuliwe dhidi yao" alisema. 

Kwa upande wake mkuu wa Majeshi Jenerali Venance Mabeyo amewataka wanajeshi kudhibiti usalama wa kambi  kwa kutoruhusu raia kukatisha  katika maeneo ya Jeshi  na kuahidi kujenga ukuta katika eneo la jeshi kambi ya Lugalo na  Mwenge na kuhiza usafi kuwa endelevu.
 Mkuu wa majeshi ya Ulinzi Tanzania jenerali,Venance Mabeyo akizungumza viongozi mbalimbali pamoja na wanajeshi la JWTZ  katika maazimisho ya miaka 54 tangu kuanzishwa kwake.
 Mbwa wa jeshi akimdhibiti adui.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...