Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
JUMUIYA ya Waanyabiashara Kariakoo imekutana na mawaziri wa watatu kutoa changmoto zao biashara wanazokutana nazo na kufanya biashara zao kuwa ngumu.

Mwenyekiti wa Mkutano huo ambaye ni Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isaac Kamwelwe amesema kuwa kukutana wa wafanyabiashara hao ni kutaka kujua changamto na kufanyia kazi ili serikali iendelee kupaata mapato.

Amesema kuwa maendeleo hayawezi kupatikana bila kuwepo kwa wafanyabiashara hivyo ni lazima kwa vongozi wenye dhamana kufanya kazi ya kukutana na wafanyabiashara kujua changamoto za biashara zinazotokana na mifumo ya kiutendaji serikalini.

Nae Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amesema kuwa wafanyabiashara wanahitajika sana katika maendeleo ya nchi kwani miradi inayotekezwa yanatokana na mapato ya ndani.

Amesema kuwa kuombaomba kunadharisha hivyo wafanyabiashara ndio nguzo ya maendeleo ikiwa ni kusoma bure kunatokana na hizo kodi ambazo ni za watanzania.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charle’s Mwijage amesema kuwa vitu vyote vilivyozuiliwa kwa ajili ya ukaguzi wa Shirika la Viwango Nchini (TBS) na Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kufanya ukaguzi bidhaa za wafabiashara kuanzi leo hadi kesho na kuma havikidhi mahitaji ya mlaji vitekezwe.

Hata hivyo Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Charles Kichere amesema kuwa kuna mchezo wa kwa wafanyabiashara wa Kariakoo kuchezea mashine za Kielektroniki ambapo wanashughulikia wote wanaofanya hivyo.

 Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isaac Kamwelwe akizungumza katika mkutano na Jumuiya ya wafanyabiashara kuhusiana na changamoto wanazokutana nazo katika biashara kupitia mamlaka za kiserikali..
 Kamishina Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) Charles Kichere akizungumza na Jumuiya ya Wafanyabiashara kuhusiana na ukusanyaji wa mapato na hatua ambazo wanazichukua kwa wafanyabiashara wasiofuata utaratibu.
  Waziri wa Fedha na Mipango Dkt Philip Mpango akizungumza na Jumuiya ya wafanyabiashara kwa kuwataka kufuata taratibu katika mamlaka zilizowekwa katika usimamiaji wa biashara hizo.
Waziri wa Viwanda biashara na uwekezaji, Charles Mwijage akizungumza na jumuiya ya wafanyabiashara jijini Dar es Salaam leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...