Na Chalila Kibuda ,Globu ya Jamii
TUME ya Vyuo Vikuu  Nchini (TCU) imetangaza maombi ya wanafunzi watakaojiunga vyuo vikuu katika mwaka wa masomo 2018/2019.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Katibu Mtendaji wa TCU Profesa Charle's Kihampa amesema kuwa jumla ya waombaji wa awamu ya kwanza walikuwa 74,113.

Amesema wanafunzi waliodahiliwa na vyuo vikuu awamu ya kwanza 43,005 katika dirisha la awamu ya kwaza. Profesa Kihampa amesema kuwa wanafunzi waliokosa kudahiliwa katika dirisha hilo ni wanafunzi 31,108.

Amesema katika uhakiki wa maombi hayo wamepata wanafunzi 39,812 ndio wenye sifa ya kujiunga na Shahada ya kwanza.

Amesema walioidhinishwa na TCU 22,743 huku waombaji 16,507 wameomba vyuo zaidi ya kimoja ambapo watatumiwa namba ya siri ya kuwa na chuo kimoja atachosoma shahada hiyo.

Kati ya maombi hayo ni wanafunzi 3,193 hawana sifa ya kujiunga na shahada ya kwanza huku waombaji waliodahiliwa miaka ya nyuma ni 562 na baadhi ya majina ya waombaji 102 yanakasoro.
Amesema dirisha la awamu ya pili litafunguliwa Septemba 6 na kufungwa Oktoba 6 mwaka huu.
Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU) Profesa Charle's Kihampa akizungumza na waandishi wa Habari kuhusiana na wanafunzi wanaopaswa kudahiliwa katika shahada ya kwanza katika mwaka masomo 2018/2019.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...