Na Humphrey
Shao, Globu ya Jamii
NAIBU Katibu
Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango ,Amina Khamis Shaban amesema hakuna sababu
yoyote ya Tasisi za Umma kuendelea kufanya Vibaya katika maeneo ya Ununuzi na Ugavi hili hali
bodi ya usimamizi wa masula hayo ipo.
Naibu katibu
Mkuu amesema hay oleo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa hotuba kwa wahitimu
wa Mahafali ya tisa ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) yaliyofanyika
katika Viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam.
“ninawaagiza
kwa kushirikiana na tasisi zingine zinazosimamia ununuzi wa Umma kama PPRA,GPSA,PPAA na zingine mlete mpango kazi
namna mtakavyofikia tasisi za umma ili kupitia Wizara ya Fedha na Mipango
tuweze kutekeleza jambo hili mapema iwezekanavyo.Lengo ni kuhakikisha tunatumia
rasilimali zilizopo ili kuleta Matokeo Makubwa kwa Wananchi” Amesema Naibu
Katibu Mkuu.
Kwa upande
wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi, Godfred
Mbanyi amesema bodi itaendelea na
jitihada zake kuhakikisha wahitimu wa fani ya ununuzi na ugavi wanakuwa na sifa
stahiki ili kuweza kupenya na kuleta ushindani katika soko la ajira la ndani nan
je ya nchi .
Mbanyi
amesema bodi imeweza kuwatafutia fursa vijana wawili wa CPSP Na Wanafunzi bora
wa somo la Procurement and Suply Audit nafasi ya ajira katika tasisi ya
Kimataifa ya Nexia SJ Tanzania ambao ni Wataalamu wa Ukaguzi, Hesabu,Kodi,
Ushauri wa Kibiashara nk.
Mbanyi
alimaliza kwa kutoa rai kwa wahitimu wote watakaotunukiwa shahada ya juu ya
fani ya ununuzi na ugavi wafanye hima kujisajili na bodi ili waweze kufanya
kazi za ununuzi na ugavi kihalali na kwa mujibu wa sheria .
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango , Amina Khamis Shaban akihutibia wakati wa mahafli ya tisa ya Bodi ya Wataalmu wa Ununuzi na Ugavi(PSPTB) Katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi , Godfred Mbanyi akitoa hotuba yake kwenye Mahafali ya tisa ya bodi hiyo.
Wahitimu wakila kiapo cha Uadilifu na Maadili mbele ya Mgeni rasmi mara baada ya kutunikiwa shahada zao mbalimbali za masuala ya Ununuzi na Ugavi katika Viwanja vya Karimjee
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango , Amina Khamis Shaban akiwa katika picha ya Pamoja na Wafanyakazi wa bodi hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...