Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye akitoa maelekezo kwa wasimamizi wa mradi wa ujenzi wa bandari kavu, Kwala eneo la Vigwaza mkoani Pwani. Wa pili kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Uhandisi, Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania Mhandisi Charles Otare na wa kwanza kulia ni Meneja wa Mradi huo kutoka SUMA JKT Raymond Kweka.
Naibu Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (aliyesimama katikati) akipata maelezo kuhusu maendeleo ya mradi wa ujenzi wa bandari kavu, Kwala mkoani Pwani kutoka kwa Mkurugenzi wa huduma za Uhandisi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania, Mhandisi Charles Ogare (anayetoa maelezo). Wa kwanza kulia ni Meneja wa Mradi huo kutoka SUMA JKT, Raymond Kweka.
Muonekano
wa eneo linaloandaliwa kujenga njia ya reli kwa ajili ya kusafirisha mizigo
inayoingia na kutoka bandari kavu, Kwala mkoani Pwani wakati wa ziara ya Naibu
Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Atashasta Nditiye (hayupo pichani)
ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...