NA WAMJW- DAR ES SALAAM.
BARAZA Tiba asili na Tiba mbadala nchini limetoa elimu kwa wakunga wa jadi kuwa kazi yao kubwa ni kuhakikisha mama mjamzito anajifungua salama kwenye kituo cha afya kilichopo karibu ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi. Hayo yamesemwa na Msajili wa Baraza la Tiba asili na Tiba mbadala nchini Dkt. Ruth Suza wakati wa semina na waandishi wa habari kuhusu umuhimu wa tiba asili na tiba mbadala nchini.
Amesema kuwa wakunga wa jadi nchini wanatakiwa kuwa kipaumbele katika kuhakikisha wamama wajawazito wanawahimiza kujifungulia katika vituo vya afya kwa usalama wa maisha ya mama na mtoto.
"Tunapita kuwaelimisha Wakunga wa jadi kuwa kazi yao kubwa ni kuhakikisha mama mjamzito anajifungua salama kwenye kituo cha afya kilichopo karibu ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi" alisema Dkt. Suza. Dkt Suza amesema jumla ya waganga wa tiba asili na tiba mbadala 19912 wamesajiliwa na Baraza la Tiba asili na Tiba mbadala nchini ili kuweza kutoa huduma hizo kwa kufuata sheria na taratibu.
Mwenyekiti wa Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala , Dk.Edmond Kayombo akizungumza na wadau mbalimbali kuhusu taratibu na hatua za usajili wa waganga,dawa na vituo vyakutolea huduma leo jijini Dar es Salaam, (kushoto ni)Msajili Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala, Ruth Suza.(Picha na Emmanuel Massaka wa MMG)
Mratibu wa Taifa tiba asili na tiba Mbadala Dkt.Liggyle Vumilia wa Wizara ya Afya akizungumza na waandishi habari na wadau mbalimbali juu hatua walizozichukua kwa watoaji huduma tiba asili na tiba mbadala leo jijini Dar es Salaam.(Picha na Emmanuel Massaka wa MMG)
Mfamasia Baraza la tiba asali na tiba Mbadala wa Wizara ya Afya, Ndahani Msigwa akizungumza na wadau mbalimbali wa afya kuhusu sheria, kanuni na taratibu za utoaji huduma za tiba mbadala leo jijini Dar es Salaam.
Sehemu wa wadau mbalimbali wakimsikiliza Mwenyekiti wa Baraza la Tiba Asili na Tiba Mbadala , Dk. Edmond Kayombo.
Picha ya pamoja
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...