Na Veronica Simba – Mtwara
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani amesema Serikali itatumia muda mwingi kadri itakavyoona inafaa ili kujiridhisha na manufaa ambayo Taifa litapata kabla ya kusaini mikataba mbalimbali ya sekta ya nishati, hususan ya mafuta na gesi. Aliyasema hayo Mtwara jana, Desemba 4 wakati akizungumza na uongozi wa Kampuni ya kigeni ya mwekezaji Maurel & Prom kutoka Ufaransa, wanaotafiti na kuchimba gesi eneo la Mnazi Bay.

Waziri Kalemani alitoa msimamo huo wa Serikali baada ya kupokea taarifa ya utendaji kazi wa kampuni hiyo iliyowasilishwa na Makamu Mkurugenzi Mkuu, Elias Kilembe, ambayo pamoja na mambo mengine, waliomba Serikali iharakishe mchakato wa utiaji saini mikataba ya uwekezaji zaidi katika sekta husika, ambayo walikwisha kuwasilisha. Akifafanua, Waziri Kalemani alisema, Serikali haikusudii kumchelewesha mwekezaji bali kinachofanyika ni kujiridhisha hatua kwa hatua, namna Taifa litakavyonufaika.

“Tutatumia muda wa kutosha kujiridhisha, hata kama ni miaka 40, lakini lazima mikataba iwe na manufaa. Huo ndiyo msimamo wa Serikali.” “Sisi tunapenda wawekezaji, tunataka waendelee kuwekeza ili tupate manufaa ya gesi na mafuta, lakini tusiibiwe,” alisisitiza.
 Wananchi wa Mtaa wa Ufukoni, Manispaa ya Mtwara wakishangilia mara baada ya Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani (kulia) kuwasha umeme katika nyumba ya mmoja wa wananchi wa eneo hilo pamoja na kuzungumza nao akiwa katika ziara ya kazi Desemba 4, 2018.
 Taswira ya sehemu ya mtambo wa kuchakata gesi asilia wa Madimba kama ilivyonaswa wakati wa ziara ya Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani Desemba 4, 2018.
 Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani (katikati-mbele) na Ujumbe wake, akikagua Mtambo wa kuchakata gesi asilia wa Madimba mkoani Mtwara, akiwa katika ziara ya kazi Desemba 4, 2018.
Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani (mwenye shati ya bluu-katikati) na Ujumbe wake, wakikagua sehemu ya mitambo ya kuchakata gesi Mnazi Bay, Mtwara alipokuwa katika ziara ya kazi, Desemba 4, 2018.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...