Na Emmnuel Masaka,Globu ya jamii
NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amewaagiza watendaji wa Halmashauri ya Kilombero kuhakikisha wavuvi wote wanasajiliwa na kuwa na vikundi ndani ya mwezi mmoja ili waweze kufanya shughuli zao na kuchangia pato la taifa.
Pia amewataka kuwaangalia wavuvi hao kama wanauhitaji wa kupata vitambulisho vya wajasiriamali alivyovitoa Rais John Magufuli wapewe ili wafanye kazi zao bila bugudha.
Akizungumza katika ziara aliyoifanya katika kijini cha Miwangani kata ya Idete wilayani humo na kutatua migogoro mbalimbali Ulega amesema kuwa wavuvi lazima wathaminiwe na kupatiwa haki zao hasa za kuwa na vikundi mbalimbali hivyo haina budi kufanya tathimini na kuwasajili ili waweze kutambulika kwani nao husaidia katika kuchangia pato la taifa.
Amesema kuwa kabla ya Januari mwakani atatembelea na kuzungumza na wavuvi hao ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kama maagizo hayo yametekelezwa vyema.
Kwa upande wao wavuvi na wafugaji wamempongeza Rais Magufuli kwa juhudi zake za kujenga Tanzania mpya na hasa kwa kuwasaidia wananchi wa kipato cha chini na wamemshukuru Waziri na Naibu waziri wa mifugo na uvuvi kwa ushirikiano wanaoutoa katika kukuza na kuimarisha sekta hiyo.
NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amewaagiza watendaji wa Halmashauri ya Kilombero kuhakikisha wavuvi wote wanasajiliwa na kuwa na vikundi ndani ya mwezi mmoja ili waweze kufanya shughuli zao na kuchangia pato la taifa.
Pia amewataka kuwaangalia wavuvi hao kama wanauhitaji wa kupata vitambulisho vya wajasiriamali alivyovitoa Rais John Magufuli wapewe ili wafanye kazi zao bila bugudha.
Akizungumza katika ziara aliyoifanya katika kijini cha Miwangani kata ya Idete wilayani humo na kutatua migogoro mbalimbali Ulega amesema kuwa wavuvi lazima wathaminiwe na kupatiwa haki zao hasa za kuwa na vikundi mbalimbali hivyo haina budi kufanya tathimini na kuwasajili ili waweze kutambulika kwani nao husaidia katika kuchangia pato la taifa.
Amesema kuwa kabla ya Januari mwakani atatembelea na kuzungumza na wavuvi hao ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kama maagizo hayo yametekelezwa vyema.
Kwa upande wao wavuvi na wafugaji wamempongeza Rais Magufuli kwa juhudi zake za kujenga Tanzania mpya na hasa kwa kuwasaidia wananchi wa kipato cha chini na wamemshukuru Waziri na Naibu waziri wa mifugo na uvuvi kwa ushirikiano wanaoutoa katika kukuza na kuimarisha sekta hiyo.
Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akizungumza na wafungaji na
wavuvi wa kijiji cha Miwangani wilaya ya Kilombero mkoa wa
Morogoro,wakati wa zaiara yake ya kuzisikiliza kero mbalimbali za
wananchi hao na kuzitafutia ufumbuzi .
Sehemu
ya Wananchi wa kijiji cha Miwangani wilaya ya Kilombero mkoa wa
Morogoro wakimsikiliza Naibu wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega
alipokuwa akizungumza nao.
Mmoja
wa Wanakijiji cha Miwangani akimshukuru Naibu Waziri wa Mifugo na
Uvuvi,Abdallah Ulega kwa kufika katika kijiji hicho na kuwatalulia kero
zao na muda mrefu.(Picha na Emmanuel Massaka,MMG)
Katibu
Tawala wa wilaya ya Kilombero,Robert Sidasela akizungumza na wafungaji
na wavuvi wa kijiji cha Miwangani wilaya ya Kilombero kuhusu kuheshimu
mipaka ya wakulima na wafungaji iliyowekwa na Serikali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...