*Wanaoishi maeneo hayo wamuangukia Waziri William Lukuvi, wamuomba aingilie kati *Diwani ajitosa kuzungumzia ukweli eneo hilo...adai wananchi wamevamia, waondoke

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

WANANCHI wa Mtaa wa Mbweni Maputo jijini Dar es Salaam wapatao 270 wamemuomba Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi kuingilia kati mgogoro wa ardhi wa eneo ambalo linadaiwa kuwa ni mali ya aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT) Daud Balali(sasa marehemu) ambalo baada ya kuwa pori na kichaka cha uhalifu waliamua kusafisha eneo hilo na kisha kuweka makazi yao.

Wakizungumza na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari leo katika eneo hilo la mtaa wa Mbweni Matupo jijini Dar es Salaam wananchi hao ambao wanadaiwa kuwa ni wavamizi wameeleza wazi kuwa ni kweli wao waliamua kusafisha eneo hilo baada ya kuwa kero kwa wananchi wa maeneo hayo ya Mbweni na walifanya hivyo baada ya kuona limekaa muda mrefu bila kuendelezwa huku wakidai wamefuatilia wizarani na kubaini halina mwenyewe kwani ni eneo ambalo halijapimwa ila wanachokiona kuna watu wameamua kutengeneza hati ili kujionesha kama wao ndio wamiliki.

Wamewaambia waandishi wa habari kutambua kuwa katika eneo hilo hadi sasa kuna watu karibu watano wamekwenda na kila mmoja anasema la kwake.Hata hivyo wananchi hao wakiomba kuoneshwa hati hakuna mwenye hati miliki huku wakidai kuwa kwa kuwa wao wanyongwe watu wenye uwezo wa kifedha wanatumia kama fimbo ya kuwanyanyasa na kutishia kwamba waondoke na kinyume na hapo nyumba zao zitabomolewa.
 Baadhi ya wananchi wa Mbweni Maputo jijini Dar es Salaam wakiwa kwenye kikao cha kuangalia namna ya kuomba msaada wa Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi kuingilia kati kwani kwa sasa wanaishi maisha ya hofu
 Mkazi wa Mtaa wa Mbweni Maputo jijini Dar es Salaam Raphael Joseph akizungumzia mgogoro wa eneo ambalo wao wameamua kufanya makazi baada ya mrefu kudai lilikuwa pori ambapo wanamuomba Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuingilia kati ili haki itendeke kwani kuna watu wanawatishia kuwaondoa  kwa nguvu
 Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Mbweni Maputo Costantine Malifa akionesha barua ya kampuni ya udalali ya Sums JKT ambayo inawataka wananchi hao kuondoka ndani ya siku 14 kuanzia jana.Hata hivyo amekataa kuitambua hiyo kwa mdaia suala la eneo hilo liko mahakamani ,hivyo hawezi kutoa usharikiano kwenye jambo analoona linakwenda kinyume na sheria
 Diwani wa Kata ya Mbweni Hashimu Mbonde(kulia)akitoa ufafanuzi kuhusu eneo hilo ambalo amedai mmiliki halali ni Anna Muganda ambaye ni mke wa aliyekuwa Havana wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT) Daud Balali ambaye kwa sasa ni marehemu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...