Na Said Mwishehe.
UONGOZI na walimu wa Shule ya Mikochen English Medium ya jijini Dar es Salaam wamepongezwa kwa kuendelea kufavya vizuri kielimu ambapo imekuwa ya pili kiwilaya, tano kimkoa na 54 kitaifa katika kundi la shule zenye watoto chini ya 40 katika mtihani wa Taifa wa darasa la saba.
Pia wamepongezwa kwa kuwandaa wanafunzi katika misingi ya dini na malezi bora wakiwamo wa hitimu wa elimu ya msingi ambao wamefanya mahafali ya grade seven ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Waziri wa Uvuvi Abdalah Ulega.
Pongezi hizo zimetolewa leo wakati wa mahafali ya shule hiyo ambapo pia viongozi na walimu wamepongezwa kwa namna wqnavyowaandaa wanafunzi katika kuhakikisha wanazingatia masomo.
Akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi Ulega, Mkurugenzi wa Utawala na Utumishi kutoka Wizara ya Kilimo na Mifugo Zacharia Kera amesema anaipongeza shule hiyo kwani imepiga hatua kimaendeleo na hasa katika kuwaandaa wanafunzo wake kitaaluma.
Wakati wa mahafali hayo wazazi na walezi wamejitokeza kwa wingi kuhakikisha wanashuhudia mahafali hayo huku mgeni rasmi akitumia nafasi hiyo kutoa pongezi pia kwa walimu waliofanikisha kuwajenga kielimu wanafunzi ambao wamehitimu shuleni hapo.
Kera amesema amefurahishwa na namna ambavyo wanafunzi wa shule hiyo wakiwamo wahitimu wa shule ya hiyo ambavyo wameandaliwa vema na kwamba wamejengwa kwenye misingi imara ya kielimu.
Mkuu
wa shule ya msingi Mikocheni English Medium, Zuwena Khamis Omar
akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika mahafali
dalasa la saba yaliyo fanika mikocheni jijini Dar es Salaam. Shule hiyo
imekuwa ya pili kiwilaya, tano kimkoa na 54 kitaifa.
Sehemu
ya wazazi na walezi wakiwa katika mahafali ya darasa la saba katika
Shule ya Mikochen English Medium iliyopo Mikocheni jijini Dar es
Salaam.
Baadhi
ya wazazi na walezi wakiwa katika mahafali ya darasa la saba
yaliyofanyika katika Shule ya Mikochen English Medium ya jijini Dar es
Salaam.
Mkurugenzi
wa Utawala wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Zacharia Kera akizungumza na
waandishi wa habari katika mahafali ya darasa la saba ya shule Mikocheni
English Medium ambapo amewataka wahitimu kuwa na nidhamu, bidii na
kutanguliza uzalendo katika yale watakayokuwa wakifanya ili kufikia
malengo yao. (Picha na Emmanuel Massaka wa MMG).
Sehemu ya wanafunzi wanaomaliza elimu ya dalasa la saba katika shule ya Mikochen English Medium iliyopo jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...