Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

SHIRIKA la Scania Tanzania imezindua kizazi kipya cha malori kwenye sekta ya usafiri nchini huku Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira na Muungano January Makamba akilisifu shirika hilo kwa kuzindua malori hayo ambayo ni marafiki wa mazingira.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi huo wa kizazi kipya cha malori ambayo mbali ya kuwa rafiki wa mazingira yemetengenezwa katika mfumo wa kuhakikisha dereva 

anakuwa salama hata inapotokea ajali pamoja na ulaji mdogo wa mafuta, Makamba amesema analipongeza Shirika la Scania Tanzania kwa kutambua dhana ya kutunza mazingira ambapo imeamua kuja na malori ambayo mfumo wake ni rafiki wa mazingira.

"Huko tunakoelekea iko haja ya kuhakikisha tunakuwa na vyombo vya usafiri ambavyo vitakuwa rafiki wa mazingira badala ya kuwa usafiri ambao unaharibu wa mazingira.Kuna baadhi ya vyombo vya usafiri vinatoa moshi mwingi ambao ni hatari kwa mazingira yetu, hivyo 

lazima tuwe na usafiri rafiki katika kuhakikusha tunakuwa salama zaidi,"amesema Makamba.Pia Makamba amesema dunia ikiwa ni pamoja na Tanzania inakaribia hatua ya kusonga mbele ambapo kuunganishwa kwa teknolojia mpya na mifano mbalimbali ya biashara inaleta ufumbuzi wa usafiri wa kudumu na utoandoa usafiri wa kawaida.
 Waziri was Nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira na Muungano January Makamba (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Scania Lars Eklund wakati wa uzinduzi wa aina mpya ya malori ya Scania jijini Dar es Salaam.Wengine ni sehemu ya maofisa wa Shirika la Scania.
 Waziri wa Nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira na Muungano January Makamba (kulia) akisalimiana na moja ya wadau wa usafiri nchini wakati wa uzinduzi wa lori la Scania 'New Generation' .Uzinduzi huo umefanyika jijini Dar es Salaam
 Waziri wa Nchi,Ofisi ya Makamu wa Rais- Mazingira na Muungano January Makamba akizungumza wakati wa uzinduzi wa malori mapya ya Shirika la Scania .Uzinduzi huo umefanyika jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Scania nchini Lars Eklund akizungumza wakati wa uzinduzi wa lori mpya ya Scania ambayo ni rafiki wa Mazingira na yenye kutumia mafuta kidogo.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais-Mazingira na Muungano January Makamba akiwa ndani ya Lori la Scania ikiwa ni ishara ya kulizindua rasmi.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...