LUSUNGU HELELA-WMU
Baada ya  malalamiko ya  Watalii walio wengi  kulazimika kuacha  vinyago kwenye viwanja vya ndege walivyokuwa wamevinunua kwenye maduka mbalimbali nchini kutokana na kukosekana kwa vibali kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania(TFS) hatimaye  Naibu Waziri na Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu ameiagiza TFS iangalie namna bora  ya kutatua tatizo hilo kwa vile limekuwa likiwaletea usumbufu watalii.

Amelibainisha hilo wakati alipokuwa akizungumza kwenye mkutano na Watumishi wa makao makuu wa Wakala wa Huduma za Misitu  Tanzania, jijini Dar es Salaam. Amefafanu kuwa  watalii wengi  hununua vinyago hivyo kwenye maduka mbalimbali hapa nchini kama zawadi ya kupeleka nchini kwao lakini  wanapofika kwenye viwanja vya ndege kwa ajili ya kusafiri navyo hudaiwa vibali vya kusafirishia  vinyago hivyo jambo ambalo huwalazimu kuviacha kutokana na usumbufu wanaoupata.

Amesema jambo hilo limekuwa likiwafanya watalii wengi kuondoka nchini wakiwa wamekasirishwa kutokana na utaratibu huo kutokuwa wazi huku wakiamini kuwa wamedhulumiwa mali yao. Amesema malalamiko hayo  sio mazuri licha ya kuwa TFS nia yake ni njema ya kuhakikisha kuwa lazima kuwe na vibali ya kusafirishia vinyago hivyo kwa ajili kuthibiti  uharibifu wa misitu.
  Naibu Waziri na Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu akizungumza na watumishi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ( TFS) wakati aliwapotembelea kwa ajili ya kuzungumza nao  ikiwa ni mara ya kwanza  tangu alipoteuliwa kushika nyadhifa hiyo.
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Dos Santos Silayo akiwasilisha taarifa kabla  Naibu Waziri na Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu  kuzungumza watumishi wa makao makuu wa  TFS, jijini Dar es Salaam.    
 Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Dos Santos Silayo akifafanua jambo kabla   Naibu Waziri na Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu kuzungumza na Menejimenti ya  TFS, jijini Dar es Salaam.
  Baadhi ya watumishi wa Wakala wa  Huduma za Misitu Tanzania ( TFS) wakimsikiliza Naibu Waziri na Maliasili na Utalii, Mhe. Constantine Kanyasu wakati ali[pokuwa akizungumza nao makao makuu ya TFS jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA LUSUNGU HELELA-MNRT)

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...