Na Mathias Canal-Wizara ya Kilimo-Arusha

Waziri wa Kilimo nchini Tanzania Mhe Japhet Hasunga amewataka mawaziri wenzake wa sekta ya Kilimo kutoka nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika Mashariki kuongeza umoja na mshikamano ili kuakisi matakwa ya jumuiya katika Uzalishaji wa bidhaa bora za Kilimo.

Waziri Hasunga ameyasema hayo Leo tarehe 7 Disemba 2018 wakati akizungumza mara baada ya kumalizika mkutano wa 12 wa Baraza la kisekta la mawaziri wa Kilimo na usalama wa chakula wa nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwemo wenyeji Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Sudani Kusini.

Mhe Hasunga alisema kuwa kadri ushirikiano mwema utakavyoendelezwa ikiwa ni pamoja na kufanya kazi kwa bidii itaimarisha tija na mafanikio ya soko la bidhaa katika jumuiya hiyo na dunia kwa ujumla.Aidha, amewataka watendaji wote katika nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki kutekeleza taarifa mbalimbali zinazoandikwa kwa ustadi mkubwa kwani kwa kiasi kikubwa kumekuwa na utekelezaji duni wa mipango hiyo.
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Katikati), Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Luhaga Mpina (Kushoto) na Waziri wa Kilimo, Mifugo, Maliasili na Utalii-Zanzibar Mhe Rashid Ally Juma wakiwa katika picha ya pamoja katika ukumbi wa mikutano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha, Leo tarehe 7 Disemba 2018. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo).
Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe Christophe Bazivamo, Waziri anayeshughulikia EAC nchini Burundi Mhe Isabelle Ndahayo, Waziri wa Kilimo nchini Kenya Mhe Mwangi Kiunjuri, Katibu Mkuu wa Kilimo nchini Rwanda Ndg Musabyimana Jean Claude, Waziri wa Kilimo Sudani Kusini Mhe Onyoti Adigo Nyikwec, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Tanzania Mhe Luhaga Mpina (Mb), Waziri wa Kilimo Tanzania Mhe Japhet Hasunga (Mb), na Waziri wa Kilimo, Mifugo, Maliasili na Utalii-Zanzibar Mhe Rashid Ally Juma wakiwa katika picha ya pamoja katika ukumbi wa mikutano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Jijini Arusha, Leo tarehe 7 Disemba 2018.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...