Na Karama Kenyunko,  globu ya jamii. 

Mnogeshaji wa video mbalimbali za wasanii (Video Queen) Rutyfiya Abubakary maarufu  'Amber Rutty’ amejikuta akiangua kulio katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya mume wake, Said Mtopali, kuanguka nje ya kizimba cha Mahakama Kufuatia kesi yao ya kufanya mapenzi kinyume na maumbile  kuahirishwa. 

Kabla ya kutokea kwa tukio hilo upande wa mashtaka ukiongozwa na wakili wa serikali Neema Bwana ulidai mbele ya Hakimu Mkazi Janet Mbando kuwa,  kesi hiyo leo January 10.2019 imekuja kwa kutajwa na upelelezi bado  haujakamilika.

 Mshitakiwa mwengine katika kesi hiyo ni James Charles maarufu kama James Delicious ambaye anakabiliwa na mashitaka ya kuchapisha video au picha za ngono  na kuzisambaza katika makundi ya mtandao wa kijamii wa WhatsApp.

Kufuatia taarifa hiyo, Hakimu Mmbando ameahirisha kesi hiyo hadi Februari 11, 2019  na washitakiwa wote wako nje kwa dhamana.

Maro baada ya kesi hiyo kuahirishwa, mshtakiwa Mtopali wakati akitoka nje ya mahakama kuanguka ghafla na kumelelwa taharuki kwa ndugu zake ambao walimnyanyua kwa haraka na kumkimbiza Hospitali kwa uchunguzi zaidi. 

Katika kesi hiyo, Amber Rutty
anadaiwa kati ya Octobar 25, mwaka huu, jijini Dar es Salaam aliimruhusu Said Mtopali kumuingilia kinyume na maumbile jambo ambalo ni kinyume na sheria.

Pia inadaiwa kati ya Octobar 25, mwaka , maeneo ya jiji la Dar es Salaam, alifanya mapenzi kinyume na maumbile na mshitakiwa Mtopali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...