Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii.

KATIKA kujenga taifa lenye mlengo wa uwajibikaji pamoja na usimamizi mzuri wa rasilimali za umma kwa manufaa kwa wote taasisi ya WAJIBU imekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu pamoja na kukuza uwajibikaji na utawala bora nchini.

Mtazamo na dhima ya taasisi ya WAJIBU vinaenda sambamba na na kasi na mlengo wa serikali wa awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais Dkt. John Magufuli ambaye amekuwa akisisitiza kuhusu uwajibikaji na utawala bora pamoja na kupiga vita masuala ya rushwa na ufisadi.

WAJIBU ni taasisi ya ya fikra ya uwajibikaji wa umma iliyoanzishwa mwaka 2015 ikiwa na malengo mbalimbali hasa kukuza uwajibikaji na utawala bora hapa nchini na kushikilia dira ya usimamizi faafu na bora zaidi wa rasilimali za umma kwa manufaa ya wote.
Taasisi ya WAJIBU imebeba dhima ya kuendelea kukua kama taasisi ya fikra ya uwajibikaji ambayo inaongeza thamani katika huduma inazotoa ili kuweza kufanikisha ustawi wa uwajibikaji na utawala bora nchini katika sekta mbalimbali za umma.

Katika kutekeleza majukumu yao taasisi ya WAJIBU inasimamia misingi ya kiutendaji na hiyo ikiwa ni pamoja na kujali watu na kuwahudumia watanzania ambao ndio walengwa wa mambo yote yanayohusu uwajibikaji na utawala bora nchini na wanaamini haki katika kuwahudumia wananchi ni moja ya msingi katika kutekeleza uwajibikaji na utawala bora.

Aidha WAJIBU ni taasisi ambayo haifungamani na upande wowote kisiasa, kijamii na kidini bali wao hutekeleza yale yanayohusu uwajibikaji pamoja na kuangalia masuala ya usawa, uvumilivu na uwazi sambamba na kuwajibika.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...