Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

Timu ya Maafisa Habari wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto pamoja na Taasisi zake iko katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya kwa kuangalia uwekezaji katika Sekta ya Afya katika kipindi cha miaka mitatu ya serikali ya Awamu ya Tano ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Akizungumza  kwenye Kampeni hiyo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Mwakilishi wa Wizara ya Afya na Meneja wa Mawasiliano na Elimu kwa Umma Gaudensia Simwanza amesema ziara hiyo katika Hospitali na Taasisi zilizo chini ya Wizara ya Afya ni kuangalia uwekezaji katika utoaji huduma bora za Afya kwa wananchi,kuhakikisha kuna nguvu kazi imara ya uzalishaji katika Sekta ya viwanda.

Amesema kuwa serikali imewekeza sehemu kubwa ya vifaa na mitambo katika hospitali na hali iliyofanya serikali kuokoa fedha nyingi kutibu wagonjwa nje ya nchi.

Simwanza amesema kuwa Hospitali ya MOI imekuwa na vifaa katika kila idara na kurahisisha utoaji huduma za Afya ambazo ni bora kutokana na Serikali kutilia mkazo uwekezaji wa vifaa tiba,mitambo, Dawa pamoja na vitendanishi.

Nae Afisa Habari wa MOI Patrick Mvungi amesema kuwa MOI itaendelea kutoa huduma bora kutokana na Serikali kuwekeza mashine mbalimbali zilizo kuwa changamoto,ambazo zilikuwa zinasababisha wagonjwa kupewa rufaa.

Mvungi ameipongeza serikali katika uwekezaji uliofanyika Hospitalini hapo pamoja na ujenzi wa majengo ya kisasa na kulaza wagonjwa kwenye 340 vitanda.Amesema katika ununuzi wa vifaa wamenunua Darubin ya kisasa ya sh.bilioni Moja.

Daktari Bingwa wa Upasuaji Moyo wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kissenge amesema serikali imenunua mtambo wa sh.Bilioni Tatu na kufanya Taasisi hiyo kuendelea kutoa huduma bora za Afya ndani na nje ya nchi.

Kissenge amesema kuwa Taasisi hiyo ni kati ya Taasisi 25 zinazotoa huduma za matibabu ya Moyo katika nchi za Afrika.Amesema magonwa ya Moyo yanatokana na wananchi kushindwa kufanya mazoezi pamoja hali ya ulaji wa vyakula.

Kissenge amesema kuwa nchi ya Thailand wananchi wake wanatumia baiskeli zaidi kuliko magari hali hiyo ni tofauti na hapa nchini ambao wanaona kutembea na magari ni ufahari. 
 Sehemu ya kufanyia  uangalizi wa magonjwa ya mwili wa binadamu kwa kutumia mitambo hiyo ambayo imenunuliwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt. John Magufuli katika Hospitali ya MOI. 
 Daktari wa Hospitali ya MOI Ngina Mitti Akizungumza na waandishi wa habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto na Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya.
Daktari Bingwa wa Picha za MRI Rahma Hingora akizungumza na waandishi wa Habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya katika Hospitali ya Mifupa (MOI) Jijini Dar es Salaam.

 Mgonjwa wa Figo Magesa Masigi akizungumza namna ya huduma za Afya zilizoboreshwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.
 Afisa Muuguzi mwandamizi wa Kitengo cha Figo Moroa Nyamatara akizungumza na waandishi wa Habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya jijini Dar es Salaam.
 Mratibu wa Maduka ya MSD Betia Kaema akizungumza na waandishi wa Habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya.
 Duka la MSD lilopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili ambalo limejngwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt John Pombe Magufuli.
 Afisa Habari wa MOI Patrick Mvungi akizungumza na waandishi habari kuhusiana na Mafanikio ya Miaka mitatu ya Rais Dkt John Pombe Magufuli katika uboreshaji wa upatikanaji wa vifaa katika Hospitali hiyo
 Jengo la MOI lilojengwa kwa udhamini wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF).
 Daktari Bingwa wa Hospitali ya MOI Hamis Shaban akizungumza na waandishi wa Habari na Timu ya Maafisa wa Habari wa Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto katika Kampeni ya Tumeboresha Sekta ya Afya.
 Meneja Uhusiano wa NHIF Akizungumza na wagojwa katika Hospitali ya MOI kuhusiana na utumiaji wa bima ya Afya katika Hospitali hiyo jijini Dar es Salaam.
 Jengo la Watoto katika Hospitali ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete ambapo limejengwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais wa Awamu ya Tano Dkt. John Pembe Magufuli.
Moja ya mtambo wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete JKCI Ulionunuliwa kwa sh.bilioni tatu katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Dkt John Pombe Magufuli.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...