Na Khadija Seif,Globu ya jamii
BENKI ya I&M imetangaza washindi watano droo ya tatu na ya mwisho promosheni ya JIDABO
Meneja Masoko na Mawasiliano
Emmanuel Kiondo amesema Kampeni ya "JIDABO na I&M Benki ilizinduliwa
mwanzoni mwa mwezi Oktoba na imedumu kwa miezi mitatu ambapo kila mwezi
washindi watano wamekua wakipatikana na kutangazwa.
Washindi watano waliopatikana leo wanafanya jumla ya idadi ya washindi wote waliopatikana katika kipindi cha miezi mitatu ya promosheni ya "JIDABO na I&M Benki" kufikia 15 ambapo kila mshindi hupata mara mbili ya akiba iliyopo kwenye akaunti yake hadi kufikia kiasi cha juu cha sh.milioni tano za " amesema Kiondo.
Hata hivyo Kiondo amefafanua jinsi vigezo vilivyopaswa mshiriki azingatie ikiwemo kufungua Akaunti ya Akiba,Akaunti ya Biashara ,Akaunti ya Mshahara,Akaunti ya mtoto katika tawi lolote la benki ya I&M katika kipindi cha promosheni.
Kwa upande wa muwakilishi kutoka Bodi ya Taifa ya Michezo ya kubahatisha Humud Abdul Hussein amesema ni muamko mkubwa kuona watanzania wengi wameshabadilisha maisha ya kupitia Michezo ya kubahatisha kama ya JIDABO na I &M Benki ambapo washindi wengi wameweza kusomesha watoto,kuendesha familia zao pamoja na biashara.
Hata hivyo ametoa pongezi kwa benki hiyo kwa kufanya promosheni hiyo na leo kufika tamati na kutangaza washindi watano waliopatikana katika droo hiyo ya mwisho wakiwemo Poulomi Joshi ,Jenipher Fredrick ,Thomas Obadia Malisa,Kefren Charles Buhongo pamoja na Kampuni ya Unisoft Technologies.
Aidha mshindi wa droo ya promosheni hiyo iliyopita ya mwezi Novemba Kennedy George amesema pesa alizoshinda ataweza kufanyia biashara zake pamoja na kumalizia ujenzi wa nyumba yake.Pia ametoa rai kwa watanzania kuwa Michezo ya kubahatisha ni michezo ambayo hakuna mtu ambae anapangwa na hakuna njia ya panya yoyote inayotumika katika kutafuta mshindi.
Washindi watano waliopatikana leo wanafanya jumla ya idadi ya washindi wote waliopatikana katika kipindi cha miezi mitatu ya promosheni ya "JIDABO na I&M Benki" kufikia 15 ambapo kila mshindi hupata mara mbili ya akiba iliyopo kwenye akaunti yake hadi kufikia kiasi cha juu cha sh.milioni tano za " amesema Kiondo.
Hata hivyo Kiondo amefafanua jinsi vigezo vilivyopaswa mshiriki azingatie ikiwemo kufungua Akaunti ya Akiba,Akaunti ya Biashara ,Akaunti ya Mshahara,Akaunti ya mtoto katika tawi lolote la benki ya I&M katika kipindi cha promosheni.
Kwa upande wa muwakilishi kutoka Bodi ya Taifa ya Michezo ya kubahatisha Humud Abdul Hussein amesema ni muamko mkubwa kuona watanzania wengi wameshabadilisha maisha ya kupitia Michezo ya kubahatisha kama ya JIDABO na I &M Benki ambapo washindi wengi wameweza kusomesha watoto,kuendesha familia zao pamoja na biashara.
Hata hivyo ametoa pongezi kwa benki hiyo kwa kufanya promosheni hiyo na leo kufika tamati na kutangaza washindi watano waliopatikana katika droo hiyo ya mwisho wakiwemo Poulomi Joshi ,Jenipher Fredrick ,Thomas Obadia Malisa,Kefren Charles Buhongo pamoja na Kampuni ya Unisoft Technologies.
Aidha mshindi wa droo ya promosheni hiyo iliyopita ya mwezi Novemba Kennedy George amesema pesa alizoshinda ataweza kufanyia biashara zake pamoja na kumalizia ujenzi wa nyumba yake.Pia ametoa rai kwa watanzania kuwa Michezo ya kubahatisha ni michezo ambayo hakuna mtu ambae anapangwa na hakuna njia ya panya yoyote inayotumika katika kutafuta mshindi.
Meneja
Masoko na Mawasiliano Emmanuel Kiondo, Benki ya I & M akiwa na
muwakilishi kutoka Bodi ya Taifa ya Michezo ya Kubahatisha Humudi Abdul
pamoja na mshindi wa droo ya mwezi novemba Kennedy George wakichezesha
droo ya pili iliyofanyika leo na kuwatangaza washindi watano wa
Promoshei ya JIDABO na I & M Bank chini ya usimamizi kutoka bodi ya
Taifa ya Michezo ya Kubahatisha.
Meneja Mauzo wa Benki hiyo I&M, Nouman Vasta kutoka Bodi ya Taifa ya Michezo yaKubahatisha akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo,wakati wa kutangaza
washindi watano walioshinda promosheni ya JIDABO na I&M benki
Meneja Masoko na Mawasiliano Emmanuel Kiondo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam wakati wa kutangaza washindi wa droo ya mwisho ya promosheni ya JIDABO na I&M benki
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...