Na Khadija Seif,Globu ya jamii
BENKI ya I&M  imetangaza washindi watano droo ya tatu na ya mwisho  promosheni ya JIDABO

Meneja Masoko na Mawasiliano Emmanuel Kiondo amesema Kampeni ya "JIDABO na I&M Benki ilizinduliwa mwanzoni mwa mwezi Oktoba na imedumu kwa miezi mitatu ambapo kila mwezi washindi watano wamekua wakipatikana na kutangazwa.

 Washindi watano waliopatikana leo wanafanya jumla ya idadi ya washindi wote waliopatikana katika kipindi cha miezi mitatu ya promosheni ya "JIDABO na I&M Benki" kufikia 15 ambapo kila mshindi hupata mara mbili ya akiba iliyopo kwenye akaunti yake hadi kufikia kiasi cha juu cha sh.milioni tano za " amesema Kiondo.

Hata hivyo Kiondo amefafanua jinsi vigezo vilivyopaswa mshiriki azingatie ikiwemo kufungua Akaunti ya Akiba,Akaunti ya Biashara ,Akaunti ya Mshahara,Akaunti ya mtoto katika tawi lolote la benki ya I&M katika kipindi cha promosheni.

Kwa upande wa muwakilishi kutoka  Bodi ya Taifa ya Michezo ya kubahatisha Humud Abdul Hussein amesema ni muamko mkubwa kuona watanzania wengi wameshabadilisha maisha ya kupitia Michezo ya kubahatisha kama ya JIDABO na I &M Benki ambapo washindi wengi wameweza kusomesha watoto,kuendesha familia zao pamoja na biashara.

Hata hivyo ametoa pongezi kwa benki hiyo kwa kufanya promosheni hiyo na leo kufika tamati na kutangaza washindi watano waliopatikana katika droo hiyo ya mwisho wakiwemo Poulomi Joshi ,Jenipher Fredrick ,Thomas Obadia Malisa,Kefren Charles Buhongo  pamoja na Kampuni ya Unisoft Technologies.

 Aidha  mshindi wa droo ya promosheni hiyo iliyopita ya mwezi Novemba  Kennedy George amesema pesa alizoshinda ataweza kufanyia biashara zake pamoja na kumalizia ujenzi wa nyumba yake.Pia ametoa rai kwa watanzania kuwa Michezo ya kubahatisha ni michezo ambayo hakuna mtu ambae anapangwa na hakuna njia ya panya yoyote inayotumika katika kutafuta mshindi.
 Meneja Masoko na Mawasiliano Emmanuel Kiondo, Benki ya I & M akiwa na muwakilishi kutoka Bodi ya Taifa ya Michezo ya Kubahatisha Humudi Abdul pamoja na mshindi wa droo ya mwezi novemba Kennedy George wakichezesha droo ya pili iliyofanyika leo na kuwatangaza washindi  watano wa Promoshei ya JIDABO na I & M Bank chini ya usimamizi kutoka bodi ya Taifa ya Michezo ya Kubahatisha.
Meneja Mauzo wa Benki hiyo I&M, Nouman Vasta kutoka Bodi ya Taifa ya Michezo yaKubahatisha akifafanua jambo kwa waandishi wa habari jijini Dar es salaam  leo,wakati wa kutangaza washindi watano walioshinda promosheni ya JIDABO na I&M benki 
 Meneja Masoko na Mawasiliano Emmanuel Kiondo  akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam wakati wa kutangaza washindi wa  droo ya mwisho ya promosheni ya JIDABO na I&M benki

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...