CHAMA tawala nchini Uganda kimemteua Rais Yoweri Kaguta Museveni kuwa mgombea wake wa urais katika uchaguzi wa mwaka 2021. Hiyo inamaana ya kuwa, kiongozi huyo mwenye miaka 74, na aliyeingia madarakani mwaka 1986, atagombea urais kwa muhula wa sita.
Taarifa ya Chama cha National Resistance Movement (NRM) kimesema katika kikao kilichoongozwa na Museveni kimesema Rais huyo aendelee kuongoza harakati za taifa kwa kugombea tena urais kwa mwaka 2021 na kuendelea ili kuondosha vikwazo vya mabadiliko na maendeleo.
Kwa mujibu wa taarifa hii iliyoandikwa na Shirika la Habari la Uingereza (BBC)linasema miaka ya nyuma Museveni aliwahi kueleza kuwa viongozi "wanaodumu" madarakani ndio chanzo cha matatizo barani Afrika.
Hata hivyo,wakati akigombea muhula wa tano wa madaraka mwaka 2016, Rais Museveni aliwahi kueleza kuwa huo haukuwa muda muafaka kwake kuondoka madarakani kwani bado alikuwa na kazi ya kufanya. CHANZO BBC.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...