Na Amisa Mussa
Jeshi La Polisi Mkoani Tabora Kwa kushirikiana na raia wema limefanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu ishirini na wawili ambao walikua wakisafiri kutoka Burundi kupitia Kigoma, Tabora kuelekea nchini Zambia wakiwa kwenye usafiri wa basi la An.
Miongoni mwa raia hao wa Burundi waliokamatwa tisa ni watoto wadogo ,ambao walikua pamoja na wazazi wao katika safari yao, raia hao wamekamatwa wakiwa wanaingia kwenye kituo kikuu cha mabasi Mjini Tabora ndani ya basi la An ambalo linafanya safari zake katika Mikoa ya Tabora na Kigoma
Kamanda wa Polisi Wilaya ya Tabora Mjini John Mfinanga, ambaye aliongoza kikosi kazi cha askari Polisi wasaidizi amesema wamefanikiwa kuwakamata raia hao wa Burundi baada ya kupata taarifa za siri juu ya ujio wao ambao walikua wakipita hapa Mkoani Tabora wakielekea nchini Zambia.
baadhi ya wananchi wameviomba vyombo vya dola kuwachukulia hatua kali za kisheria mawakala ambao wanawasafirisha wahamiaji haramu kutoka nchi jirani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...