Kururunfa kata,  huko Okinawa,Japan. 
 Shihan Magoma na sensei Rumadha Fundi 1980 Zanaki Dojo, maadhimisho ya miaka 7 ya Goju Ryu Jundokan Tanzania.
Shishochin kata, Okinawa, Japan 


Baada ya kumaliza kongamano la maadhimisho ya miaka 65 ya chama cha Goju Ryu Karate -Do Jundokan mwezi wa November mwaka 2018 huko Tomigusuku, Okinawa, Japan, sensei Rumadha Fundi na wenzie washiriki toka nchi zaidi ya 25 walitembelea makumbusho ya sanaa ya Karate iliyomo ndani ya ukumbi maalum kwa shughuli za karate. Ukumbi huo maarufu wa  " Okinawa Karate Kaikan" ulifunguliwa miaka michache na mfalme Akihito wa japan kwa lengo la kuwa na maadhimisho ya michezo ya Karate visiwani humo.

Mambo mengi muhimu katika ziara hiyo ilikuwa pia kuona vitabu na video mbalimbali za waasisi wa mchezo wa karate kabla hata karate kuwa imebuniwa mnamo karne ya 18,ikiwa ni mafunzo ya siri na ikiwa imegawanywa katika vitongoji vitatu vya visiwani hapo. Utamaduni huo wa Okinawa wa sanaa hii wakati huo ilikuwa unaitwa " Te", ikimaanisha mkono. Hivyo ndivyo kila kitongoji kimoja kati hivyo vitatu yaani hiyo miji ya Shuri, Tomari na Naha ikajipatia sanaa ya kujilinda kwa majina ya, Shuri-Te, Tomari-Te, na Naha-Te

SHURI-TE:
Watu muhimu sana katika mchango wa sanaa ya Karate huko Okinawa na huenda watu na mashabiki wengi wa Karate hawamfahamu, ni mwalimu aitwae Matsumura Sokon, alifundisha magwiji wengi waliokuja baadae kuanzisha mitindo mingi sana ya Karate huko Okinawa. 

Baadhi ya walimu maarufu na niwanafunzi wa Matsumura Sokon ( Alijifunza sanaa ya kujilinda toka kwa Sakugawa Kanga), ni:Anko Asato, Anko Itosu  (mpaka hii leo anajulikana kama baba wa karate ya kisasa ), moja ya wanafunzi wa Itosu ni Gichin Funakoshi wa Shotokan, Chotoku Kyan ( Kachangia sana mtindo wa Shorin Ryu), Choshin  Chibana ( mwanzilishi wa mtindo wa Shorin Ryu), na Gichin Funakoshi( Mwanzilishi wa mtindo wa Shotokan),  ambae aliendelea na mafunzo chini ya Anko Itosu. Pia vile vile yupo mwengine ambae ni mwanafunzi wa Matsumura Sokon, anaitwa Kenwa Mabuni na Tatsuo Shimabuku ( Mwanzilishi wa mtindo wa Isshin Ryu).

Mitindo ya sasa ya Karate iliyozaliwa na ushawishi wa misingi ya Shuri-Te ni: Shotokan, Wado Ryu, Motobu Ryu, Shorin Ryu, Shudokan, na Shorinji Ryu ( Mtindo uliobuniwa na Sakugawa Kanga, mwalimu wa Matsumura Sokon).

TOMARI-TE:
Chanzo cha sanaa hii ni kitongoji cha Tomari ambayo ni bandari kuu kisiwani hapo tokea mnamo karne ya 17. Walimu muhimi toka hapo walikuwa ni:

Kosaku Matsumura, Motobu Choki (Mwanzilishi wa Motobu Ryu), Yamazato Gikei, Kyan Chotoku ni baadhi ya walimu waliokuwa wanajifunza sanaa za vitongoji zaidi ya kimoja.

Mitindo iliyozaliwa chini ya ushawishi wa Tomari-Te ni: Motobu Ryu, Shorinji Ryu, Matsubayashi Ryu, na Gohaku kai. Hapo mitindo iliyorudiwa mara mbili inamaanisha waasisi hao walijifunza pande zote mbili za miji hito ya Okinawa.

NAHA-TE.
Kabla ya vita kuu ya pili ya duania, mji wa Naha ulikuwa ndio mjimmaarufu wa biashara katika visiwa vya Ryu Kyu. Hivyo ndivyo uliwavutia wafanya biashara wengi toka China . Hivyo ndivyo sanaa ya Naha-Te ilikuwa na ushawishi mwingi wa mbinu toka kusini mwa China hasa kwa mbinu za "Fujian White Cranes Systems". 

Kulikuwa na msongamano mkubwa wa wahamiaji wa kibiashara wa China katika mji wa Naha. Mtu ambaye alikwenda China kujifunza mbinu hizo za kichina na baadae kurudi Okinawa , alikuwa mwalimu Karyo Higaonna ambaye ndio kiini kikubwa cha kuiunganisha sanaa ya Kichina na Naha-Te mnamo moaka ya 1880.

Baadhi ya walimu wachache maarufu toka mji wa Naha ni:

Karyo Higaonna (Mwalimu wa Chojun Miyagi), Chojun Miyagi (Mwanzilishi wa mtindo wa Goju Ryu) ambaye pia alikwenda China ya kusini kujifunza sanaa za Kichina, Kyoda Juhatsu, Kenwa Mabuni (Mwanzilishi wa mtindo wa Shito Ryu), na Uechi Kanbun (Mwanzilishi wa mtindo wa Uechi Ryu).
Mitindo ya  karate iliyozaliwa chini ya ushawishi wa Naha-Te ni:
Okinawa Goju Ryu, Uechi Ryu na Shito Ryu.

Pia vilevile kwa manufaa ya kuwaelimisha wanakarate wa cha na historia za Kata mitindo tofauti, napenda vilevile kusitaja kata hizo na kimbuko lake kila moja.

Kata za Shuri-Te ni : Naihanchi, Pinan, Kusanku, Passai, Jion, Jitte, Rohai, Chinto na Gojushisho.

Kata za  Tomari-Te ni:Naihanchi, Rohai, Passai, Wankan, Wansu na Sesan.
Kata za Naha -Te ni : Sanchin, Saifa, Seiyunchin, Shisochin, Seipai, Seisa, Tensho, Kururunfa, na Suparinpei.

Nakala hii imenukuliwa na Sensei Rumadha Fundi toka makumbusho ya Karate katika "Okinawa Karate Kaikan”, huko Tomigusuku, Okinawa, Japan.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...