Mkazi wa jijini Dar es Salaam, Yahaya Hassan Makolija, leo amekabidhiwa fedha zake jumla ya shilingi milioni 10 alizoshinda kwenye bahati nasibu ya Biko inayotesa katika viunga vya nchi yetu.

Makabidhiano hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam na kuongozwa na Mratibu wa Matukio wa Biko Hassan Melles, ambapo katika droo ya jana Jumapili, wengine pia waliibuka na bodaboda na mamilioni kutoka Biko. 

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Makolija aliishukuru Biko kwa kumkabidhi fedha zake akisema kuwa itamsaidia kwa kiasi kikubwa katika maisha yake ya kila siku.

Kucheza Biko sasa ni kuanzia sh 500 na sh 1000 na kuendelea, huku ushindi wake ukianzia sh 1000 hadi sh 100000 kwa watakaocheza sh 500 hadi sh 9500 wakati  watakaocheza kwa sh 1000 na kuendelea, mchezaji anaweza kujishindia zawadi ya papo kwa hapo kuanzia sh 5000 hadi sh milioni moja bila kusahau wote kuingia kwenye droo kubwa ya Jumatano na Jumapili.

Bahati nasibu ya Biko inachezwa kwa mitandao ya simu minne ambayo ni Tigo Pesa, M-Pesa, Artel Money na HaloPesa, ambapo namba ya Kampuni ni 505050 na kumbukumbu namba 2456, huku Watanzania wakiweza kujishindia zawadi kubwa katika droo ya Jumatano na Jumapili.
 Yahaya Makolija akiwa na shangwe kubwa baada ya kukabidhiwa sh million 10 alizoshinda kutoka kwenye droo kubwa ya Bahati nasibu ya Biko iliyofanyika juzi Jumapili jijini Dar es Salaam. Droo nyingine kubwa hufanyika kila Jumatano na Jumapili bila kusahau zawadi za papo kwa hapo zinazoenda kwa washindi kila wakati. 
Mshindi wa sh milioni 10 wa droo ya 182 wa bahati nasibu ya Biko, Yahaya Hassan Makolija, kulia akipokea fedha zake kwa furaha kubwa kutoka kwa Mratibu wa matukio wa Biko, Hassan Melles, katika makabidhiano yaliyofanyika jana jijini Dar es Salaam ikiwa siku moja tu baada ya kuibuka na ushindi kwenye droo iliyofanyika Jumapili, ambapo droo hizo kubwa hufanyika kila Jumatano na Jumapili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...