Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imekana kuhusika na matangazo ya kihalifu ya ajira yaliyosambazwa maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Katika taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi Dkt. Athumani Kihamia, NEC ameutaarifu umma kuwa haihusiki na matangazo hayo yenye lengo la kuwatapeli wananchi kuwa, Tume imetoa ajira za muda.

Dkt. Kihamia alifafanua kuwa kutokana na tangazo hilo, wananchi walioomba ajira hizo wamekuwa wakiambiwa watoe kiasi cha fedha kwa madai kuwa ni kwa ajili ya mafunzo.

“Hatua kali za Kisheria zitachukuliwa dhidi ya mtu au kundi la watu wanaotumia au wanaopanga kutumia jina la Tume ya Taifa ya Uchaguzi kufanya vitendo vya kihalifu” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.

Katika taarifa yake, Dkt. Kihamia aliwasihi wananchi kuendelea kutoa taarifa mara tu wanapohisi uwepo wa watu au kundi la watu wenye nia mbaya ya kulichafua jina la Tume yaTaifa yaUchaguzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...