Mkuu wa wilaya ya Monduli Idd Kimanta akihutubia siku ya wafanyakazi duniani mkoani Arusha,ambapo alimuwakilisha mkuu wa mkoa Mrisho Gambo.
Maandamano ya wafanyakazi kama yanavyoonekana pichani Jijiji Arusha.
Maandamano yakiendelea kuelekea katika uwanja wa Shekhe Amri Abeid Karume Jijiji Arusha.




Na Vero Ignatus,Arusha

Mkuu wa Wilaya ya Monduli Iddi Kimanta amekenea vikali tabia ya baadhi ya Waajiri wakorofi wanaowanyanyasa Wafanyakazi wao na kuwataka Viongozi wa vyama vya Wafanyakazi kuwachukulia hatua mapema pale watakapobainika.

Amesema hayo wakati akitubia katika Siku ya Wafanyakazi mkoani Arusha akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Arusha ambapo Mrisho Gambo ambapo amewataka waajiri wajiepushe na vitendo vya unyanyasaji kwani sheria itafuata mkondo wake.

"Hatutamfumbia macho baadhi ya waajiri wakorofi wanaowanyanyasa wafanyakazi wao vyama vyavwafanyakazi fanyeni jitihada kuwabaini ili wachukuliwe hatua kali za kisheria.alisema Kimanta.''

Mhe.Kimanta amewataka Viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi kutatua kero za wafanyakazi badala ya kusubiri siku ya wafanyakazi na kutoa kero zao.

Nae Mwenyekiti wa shirikisho la vyama vya Wafanyakazi mkoani Arusha (TUCTA) Lota Laizer ameiomba serikali itoe nyongeza ya mishahara pamoja na ongezeko la asilimia la 1 la kila mwaka kama ilivyo matakwa ya sheria.

Aidha Laizer amewataka Wafanyakazi kuwa viongozi wa kisiasa wanatekeleza majukumu yao bila kukiuka sheria za wafanyakazi na kutumia lugha za kuwadhalilisha wafanyakazi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...