Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro Bw. Yefred Myenzi, akizungumza na wandishi wa Habari ofisini kwake kuhusu kilimo cha umwagiliaji. pamoja na mambo mengine kinavyochangia katika pato la Halmashauri hiyo pamoja na kubadilisha Maisha ya wananchi wa Wilaya hiyo.


NA MWANDISHI MAALUM – SIMANJIRO

IMEELEZWA kuwa kilimo cha  umwagiliaji  ni chanzo kikubwa cha mapato katika Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro kwani huingiza  shilingi Milioni mia moja  ishirini (120) hadi milioni miambili (200) kwa mwaka na kuinua  pato la wananchi  wilayani humo.

 Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi  Mtendaji  wa Halmashauri hiyo Bwana Yefred Myenzi  ambapo amesema serikali ilitoa kiasi cha takribani shilingi Bilioni 2.2 kwa ajili ya ujenzi na maboresho ya skimu zaa umwagiliaji sambamba na kuwawezesha wakulima kupata elimu ya kilimo, uendeshaji na matunzo ya miundombinu ya  umwagiliaji jambo ambalo limepelekea wanachi kujikita zaidi kwenye kilimo  cha umwagiliaji  na kuongeza pato la Halmashauri,

“Mazao mengi yanayolimwa katika skimu za umwagiliaji ni mpunga  na mazao menginge ya Mboga mboga, lakini pia kuna mazao ambayo hayalimwi katika skimu hizo kama vile Matama, Uwele na Shayiri zao ambalo linatumika kama malighafi katika viwanda vingi vya beer nchini.” Alisema Bw. Myenzi

Bw. Myenzi alisema kuwa Skimu hizo zimesaidia kuwepo na chakula cha kutosha na Usalama wa chakula katika Wilaya hiyo, Pamoja na kwamba Kilimo hicho kinakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwa na pamoja na skimu hizo kuwa mbali na masoko jambo ambalo linapelekea kupanda kwa gharama za usafishaji wa mazao kwenda kwenye masoko  na kukosekana kwa bei ya uhakika kitendo ambacho kinamuumiza mkulima pamoja na kukosekana kwa vinu vya kuchakata        nafaka jambo ambalo linapelekea kukosekana kwa chakula cha mifugo kitokanacho na mabaki ya nafaka hizo.

Awali akiongea katika kikao hicho kabla ya kutembelea skimu hizo za umwagiliaji, Mhandisi wa kanda ya Umwagiliaji Dodoma inayohusisha mikoa ya Dodoma, Singida na Simanjiro Bi Lucy Lema, alisema kuwa kutokana na kilimo cha umwagiliaji  kuwa chenye tija kwa kuongeza pato la taifa na kuwepo kwa  uhakika wa chakula nchini, Serikali ina mikakati kabambe ya kuendeleza kilimo hicho kwa kufanya upanuzi wa maeneo  na kufanya  tafiti  kabla ya ujenzi wa mabwawa, kufanyia ukarabati wa Miundombinu ya umwagiliaji na kuendeleza skimu ndogo ndogo za umwagiliaji kupitia miradi mbali mbali.
                                                                  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...