Anaripoti dixonbusagaga

Baadhi ya wasafirishaji wa Dawa za kulevya aina ya Mirungi wamepambana na askari Polisi katika eneo la Sadala wilayani Hai wakigombea  Gunia la kilogramu 50 za dawa hizo zilizokamatwa wakati zikisafirishwa kuelekea Arusha.

Tukio hilo limetokea majira ya saa nane za usiku katika eneo hilo ambapo pikipiki iliyokuwa imebeba mzigo wa Mirungi  ikiendeshwa na mmoja ya vijana hao ilipata ajali  kisha mhusika  alikimbia na kutelekeza  pikipiki na gunia hilo la Mirungi

Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,ACP Hamisi Issah alithibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akieleza kuwa katika tukio hilo Polisi wamefanikiwa kukamata mtuhumiwa mmoja aliyemtaja kwa jina la Stephano John (17) mkazi wa Bomang’ombe ,kilogramu 50 za Dawa za kulevya aina ya Mirungi pamoja na pikipiki mbili.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...