Anaripoti dixonbusagaga
Baadhi ya wasafirishaji wa Dawa za kulevya aina ya Mirungi
wamepambana na askari Polisi katika eneo la Sadala wilayani Hai wakigombea Gunia la kilogramu 50 za dawa hizo
zilizokamatwa wakati zikisafirishwa kuelekea Arusha.
Tukio hilo limetokea majira ya saa nane za usiku katika eneo
hilo ambapo pikipiki iliyokuwa imebeba mzigo wa Mirungi ikiendeshwa na mmoja ya vijana hao ilipata
ajali kisha mhusika alikimbia na kutelekeza pikipiki na gunia hilo la Mirungi
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro ,Kamishna Msaidizi wa
Polisi ,ACP Hamisi Issah alithibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akieleza
kuwa katika tukio hilo Polisi wamefanikiwa kukamata mtuhumiwa mmoja aliyemtaja
kwa jina la Stephano John (17) mkazi wa Bomang’ombe ,kilogramu 50 za Dawa za
kulevya aina ya Mirungi pamoja na pikipiki mbili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...