HIVI Karibuni Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), lilifanya Maadhimisho ya Miaka 50. Ambapo mgeni rasmi katika Maadhimisho hayo alikuwa Mh. Majaliwa Kassimu Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye aliwakilishwa na Waziri Ofisi ya Waziri Mkuuu- Uwekezaji Mhe. Angela Jasmine Kairuki. Pamoja na Maadhimisho hayo, TPDC ilitoa TUZO kwa baadhi ya WASTAAFU waliokuwa na michango mbalimbali katika utumishi wao. Pichani juu Bi Marie Msellemu, MKUU wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano, kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi wa TPDC, akimkabidhi Prof. Mark Mwandosya TUZO ya kuutambua mchango wake mkubwa kwa TPDC kwa nafasi yake kama Kamishna wa kwanza wa Petroli nchini na Mwenyekiti wa BODI ya Shirika la TPDC katika utumishi wake.
Picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...