Na Vero Ignatus, Arusha
Nchi za Tanzania na Kenya wamezindua zoezi rasmi la kupima utayari kama nchi za Afrika ya Mashariki wa kukabiliana na magonjwa ya kuambukiza kama homa ya bonde la Ufa na Ebola.

Waziri wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu amesema jambo kubwa watakaloliangalia katika zoezi hilo ni pamoja na kuona kama vipo vifaa tiba vya kutosha endapo umetokea mlipuko wa magonjwa hayo.

Tunaangalia kama wataalamu wetu wanaao ujuzi wa kuwahudumia wagonjwa au kuzuia ugonjwa usienee kwa watu na kwa wanyama wengi zaidi ikianguka ebola Tanzania Kenya haitakuwa salama.ikianguka leo Ebola Tanzania ,Kenya haipo salama kwasababu tunapakana na nchi ambayo sasahivi inamlipuko wa ugonjwaa wa EBOLA ambayo ni Jamuhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Waziri Mwalimu amesema serikali inayo mikakati na mipango ya kuweza kukabiliana na magonjwa hayo ya bonde la ufa ambapo zoezi hili litatoa picha halisi kuwa kama upo utayari kiasi gani kupambana au kukabiliana na magonjwa hayo ya bonde la Ufa.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amesema Wizara ipo makini katika jambo kutokana na swala la kiasili kwamba magonjwa yanayotoka kwa wanyama pori kwa mifugo ambayo inafugwa majumbani.

Amesema kupitia vituo vya vilivyopo katika mipaka na vile vilivyopo katika mikoa ya mipakani vina wataalam wa kutosha ambao wanaweA kushughulika na kutambua linapoibuka tatizo.

Mathalani ugonjwa wa kimeta na kwa bahati njema sana ugonjwa kama huu sisi wenyewe kama nchi tunao uwezo tunatengeneza dawa za kukinga na magonjwa haya kupitia taasisi yetu ya TVLA iliyopo Kibaha.

Amesema Wizara ya mifugo ni sehemu ya mkakati huo wa Afya moja ambao unasimamiwa na ofisi ya waziri mkuu , na wamekumuika ya Sekretarieti ya EAC kwaajili ya kuhakikisha kuwa mradi huo wa kusimamia magonjwa yanayoweza kuambukiza binadamu na wanyama kutoka eneo moja kwenda jingine tunashiriki kikamikifu kuyazuia.

Amesema wanachohangaikia kwa sasa ni utayari wa mataifa haya katika kupambana na maradhi ya bonde la ufa.

Amewatoa hofu wananchi na kusema kuwa wataalamu katika nchini ya Tanzania wapo tayari wanashirikiana na wafugaji ambapo mifugo inakaguliwa mara kwa mara na itakapogundulika tatizo kwamba.
Waziri wa Afya maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto  Ummy Mwalimu akizungumza katika uzinduzi wa zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Bonde la Ufa.

Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akizungumza katika uzinduzi wa zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Bonde la Ufa.
Waziri wa Afya maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto Mhe.Ummy Mwalimu akiwa na Adan Mohamed Naibu Katibu mkuu wa EAC anayeshughulikia sekta ya huduma na uzalishaji wakifuatilia maswali mbalimbali kutoka kwa waandishi wa habari wa nchiji Kenya na Tanzania.
Baadhi ya viongozi kutoka Jumuiya ya Afrika ya Mashariki akiongozwa na Adan Mohamed Naibu Katibu mkuu wa jumuiya ya Afrika ya Mashariki anayeshughulikia sekta ya huduma za uzalishaji Waziri wa Afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu, Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi  Abdallah Ulega akizungumza katika uzinduzi wa zoezi la utayari wa kukabiliana na ugonjwa wa Bonde la Ufa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...