Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
Azam FC imefanikiwa kutinga fainali ya Kombe la Kagame kwa mara ya tatu mfululizo baada ya kuwaondosha kwa mikwaju ya penati As Maniema Union ya DR Congo.
Mchezo huo uliokuwa wa kasi na ushindani, ilichukua dakika 120 kuweza kupatikana kwa mshindi atakayeenda kucheza na KCCA ya Uganda kwenye mchezo wa fainali.
Azam ambao ndio mabingwa watetezi wakiwa wamelichukua mara mbili mfululizo watacheza fainali ya nne kihistoria siku ya Jumapili.
Katika Mikwaju ya Penati, Azam walifanikiwa kufunga penati 5-4 kufuatia dakika 120 kumalizika kwa suluhu.
Mabingwa hao watetezi wa michuano hiyo mara mbili mfululizo, watacheza fainali hiyo dhidi ya KCCA ya Uganda Jumapili hii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...