Timu ya Taifa ya Algeria imefanikiwa kutwaa ubingwa wa mataifa huru Afrika AFCON baada ya kuifunga Senegal kwa goli 1-0.

Algeria wanabeba ubingwa huo kwa mara ya pili baada ya miaka 29 toka ilivyochukua kwa mara ya kwanza huku Senegal akiwa hajalibeba hata moja.

Mchezo huo ulianza na kasi ilichukua dakika 2 kwa Algeria kuandika goli la kuongoza kupitia kwa mshambuliaji wake Baghdad Bounedjah baada ya kupiga mpira na kumgonga beki wa Senegal na kupoteza mwelekeo wa mpira.

Mchezo ulikuwa na kasi kubwa, Senegal wakisaka goli la kusawazisha huku Algeria wakitaka kupata uhakika zaidi wa ushindi kwa kupata goli.

Mpaka mapumziko Algeria walienda vyumbani wakiwa kifua mbele. Kipindi cha pili kilianza kwa kasi na washambuliaji wa Senegal kushindwa kutumia nafasi walizozipata.

Mpaka dakika 90 zinamalizika Algeria wanatwaa ubingwa kwa mara ya pili baada ya muda mrefu.

Mchezaji Ismael Benaccer wa Algeria amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa AFCON mwaka huu huku Mlindamlango wa Algeria Rais Mbolhi ndiyo Golikipa bora wa AFCON.

Algeria wamefanikiwa kuruhusu nyavu zao kutikishwa mara 2 dhidi ya Nigeria mchezo uliomalizika kwa ushindi wa 2-1 na ule wa Ivory Coast 1-1 ulioamuliwa kwa mikwaju ya penati na wakifunga jumla ya 13.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...